إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ
Itha ashshamsu kuwwirat
Jua litakapo kunjwa,
The Overthrowing
إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ
Itha ashshamsu kuwwirat
Jua litakapo kunjwa,
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتْ
Wa-itha annujoomu inkadarat
Na nyota zikazimwa,
وَإِذَا ٱلْجِبَالُ سُيِّرَتْ
Wa-itha aljibalu suyyirat
Na milima ikaondolewa,
وَإِذَا ٱلْعِشَارُ عُطِّلَتْ
Wa-itha alAAisharu AAuttilat
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
وَإِذَا ٱلْوُحُوشُ حُشِرَتْ
Wa-itha alwuhooshu hushirat
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
وَإِذَا ٱلْبِحَارُ سُجِّرَتْ
Wa-itha albiharu sujjirat
Na bahari zikawaka moto,
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتْ
Wa-itha annufoosu zuwwijat
Na nafsi zikaunganishwa,
وَإِذَا ٱلْمَوْءُۥدَةُ سُئِلَتْ
Wa-itha almawoodatu su-ilat
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
بِأَىِّ ذَنۢبٍ قُتِلَتْ
Bi-ayyi thanbin qutilat
Kwa kosa gani aliuliwa?
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتْ
Wa-itha assuhufunushirat
Na madaftari yatakapo enezwa,
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتْ
Wa-itha assamao kushitat
Na mbingu itapo tanduliwa,
وَإِذَا ٱلْجَحِيمُ سُعِّرَتْ
Wa-itha aljaheemu suAAAAirat
Na Jahannamu itapo chochewa,
وَإِذَا ٱلْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ
Wa-itha aljannatu ozlifat
Na Pepo ikasogezwa,
عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّآ أَحْضَرَتْ
AAalimat nafsun ma ahdarat
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلْخُنَّسِ
Fala oqsimu bilkhunnas
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
ٱلْجَوَارِ ٱلْكُنَّسِ
Aljawari alkunnas
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
وَٱلَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ
Wallayli itha AAasAAas
Na kwa usiku unapo pungua,
وَٱلصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Wassubhi ithatanaffas
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ
Innahu laqawlu rasoolin kareem
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
ذِى قُوَّةٍ عِندَ ذِى ٱلْعَرْشِ مَكِينٍ
Thee quwwatin AAinda theealAAarshi makeen
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
مُّطَاعٍ ثَمَّ أَمِينٍ
MutaAAin thamma ameen
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍ
Wama sahibukum bimajnoon
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
وَلَقَدْ رَءَاهُ بِٱلْأُفُقِ ٱلْمُبِينِ
Walaqad raahu bilofuqialmubeen
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلْغَيْبِ بِضَنِينٍ
Wama huwa AAala alghaybi bidaneen
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَـٰنٍ رَّجِيمٍ
Wama huwa biqawli shaytaninrajeem
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ
Faayna tathhaboon
Basi mnakwenda wapi?
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَـٰلَمِينَ
In huwa illa thikrun lilAAalameen
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ
Liman shaa minkum an yastaqeem
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Wama tashaoona illa anyashaa Allahu rabbu alAAalameen
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.