عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
AAabasa watawalla
Alikunja kipaji na akageuka,
He Frowned
عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
AAabasa watawalla
Alikunja kipaji na akageuka,
أَن جَآءَهُ ٱلْأَعْمَىٰ
An jaahu al-aAAma
Kwa sababu alimjia kipofu!
وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Wama yudreeka laAAallahu yazzakka
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكْرَىٰٓ
Aw yaththakkaru fatanfaAAahu aththikra
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
أَمَّا مَنِ ٱسْتَغْنَىٰ
Amma mani istaghna
Ama ajionaye hana haja,
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
Faanta lahu tasadda
Wewe ndio unamshughulikia?
وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Wama AAalayka alla yazzakka
Na si juu yako kama hakutakasika.
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسْعَىٰ
Waamma man jaaka yasAAa
Ama anaye kujia kwa juhudi,
وَهُوَ يَخْشَىٰ
Wahuwa yakhsha
Naye anaogopa,
فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ
Faanta AAanhu talahha
Ndio wewe unampuuza?
كَلَّآ إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ
Kalla innaha tathkira
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Faman shaa thakarah
Basi anaye penda akumbuke.
فِى صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ
Fee suhufin mukarrama
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍۭ
MarfooAAatin mutahhara
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
بِأَيْدِى سَفَرَةٍ
Bi-aydee safara
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
كِرَامٍۭ بَرَرَةٍ
Kiramin barara
Watukufu, wema.
قُتِلَ ٱلْإِنسَـٰنُ مَآ أَكْفَرَهُۥ
Qutila al-insanu ma akfarah
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
مِنْ أَىِّ شَىْءٍ خَلَقَهُۥ
Min ayyi shay-in khalaqah
Kwa kitu gani amemuumba?
مِن نُّطْفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Min nutfatin khalaqahu faqaddarah
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Thumma assabeela yassarah
Kisha akamsahilishia njia.
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقْبَرَهُۥ
Thumma amatahu faaqbarah
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Thumma itha shaa ansharah
Kisha apendapo atamfufua.
كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَآ أَمَرَهُۥ
Kalla lamma yaqdi maamarah
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَـٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Falyanthuri al-insanuila taAAamih
Hebu mtu na atazame chakula chake.
أَنَّا صَبَبْنَا ٱلْمَآءَ صَبًّا
Anna sababna almaasabba
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
ثُمَّ شَقَقْنَا ٱلْأَرْضَ شَقًّا
Thumma shaqaqna al-arda shaqqa
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
فَأَنۢبَتْنَا فِيهَا حَبًّا
Faanbatna feeha habba
Kisha tukaotesha humo nafaka,
وَعِنَبًا وَقَضْبًا
WaAAinaban waqadba
Na zabibu, na mimea ya majani,
وَزَيْتُونًا وَنَخْلًا
Wazaytoonan wanakhla
Na mizaituni, na mitende,
وَحَدَآئِقَ غُلْبًا
Wahada-iqa ghulba
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
وَفَـٰكِهَةً وَأَبًّا
Wafakihatan waabba
Na matunda, na malisho ya wanyama;
مَّتَـٰعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَـٰمِكُمْ
MataAAan lakum wali-anAAamikum
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Fa-itha jaati assakhkha
Basi utakapo kuja ukelele,
يَوْمَ يَفِرُّ ٱلْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ
Yawma yafirru almaro min akheeh
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Waommihi waabeeh
Na mamaye na babaye,
وَصَـٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Wasahibatihi wabaneeh
Na mkewe na wanawe -
لِكُلِّ ٱمْرِئٍ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ
Likulli imri-in minhum yawma-ithinsha/nun yughneeh
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ مُّسْفِرَةٌ
Wujoohun yawma-ithin musfira
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
ضَاحِكَةٌ مُّسْتَبْشِرَةٌ
Dahikatun mustabshira
Zitacheka, zitachangamka;
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌ
Wawujoohun yawma-ithin AAalayhaghabara
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ
Tarhaquha qatara
Giza totoro litazifunika,
أُو۟لَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلْكَفَرَةُ ٱلْفَجَرَةُ
Ola-ika humu alkafaratu alfajara
Hao ndio makafiri watenda maovu.