وَٱلنَّـٰزِعَـٰتِ غَرْقًا
WannaziAAati gharqa
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
Those who drag forth
وَٱلنَّـٰزِعَـٰتِ غَرْقًا
WannaziAAati gharqa
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
وَٱلنَّـٰشِطَـٰتِ نَشْطًا
Wannashitati nashta
Na kwa wanao toa kwa upole,
وَٱلسَّـٰبِحَـٰتِ سَبْحًا
Wassabihati sabha
Na wanao ogelea,
فَٱلسَّـٰبِقَـٰتِ سَبْقًا
Fassabiqati sabqa
Wakishindana mbio,
فَٱلْمُدَبِّرَٰتِ أَمْرًا
Falmudabbirati amra
Wakidabiri mambo.
يَوْمَ تَرْجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Yawma tarjufu arrajifa
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
تَتْبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
TatbaAAuha arradifa
Kifuate cha kufuatia.
قُلُوبٌ يَوْمَئِذٍ وَاجِفَةٌ
Quloobun yawma-ithin wajifa
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
أَبْصَـٰرُهَا خَـٰشِعَةٌ
Absaruha khashiAAa
Macho yatainama chini.
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِى ٱلْحَافِرَةِ
Yaqooloona a-inna lamardoodoona feealhafira
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
أَءِذَا كُنَّا عِظَـٰمًا نَّخِرَةً
A-itha kunna AAithamannakhira
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
قَالُوا۟ تِلْكَ إِذًا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌ
Qaloo tilka ithan karratun khasira
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌ وَٰحِدَةٌ
Fa-innama hiya zajratun wahida
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Fa-itha hum bissahira
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Hal ataka hadeethu moosa
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
إِذْ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلْوَادِ ٱلْمُقَدَّسِ طُوًى
Ith nadahu rabbuhu bilwadialmuqaddasi tuwa
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
ٱذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Ithhab ila firAAawna innahu tagha
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Faqul hal laka ila an tazakka
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ
Waahdiyaka ila rabbika fatakhsha
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
فَأَرَىٰهُ ٱلْـَٔايَةَ ٱلْكُبْرَىٰ
Faarahu al-ayata alkubra
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Fakaththaba waAAasa
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ
Thumma adbara yasAAa
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Fahashara fanada
Akakusanya watu akanadi.
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلْأَعْلَىٰ
Faqala ana rabbukumu al-aAAla
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلْـَٔاخِرَةِ وَٱلْأُولَىٰٓ
Faakhathahu Allahu nakalaal-akhirati wal-oola
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَعِبْرَةً لِّمَن يَخْشَىٰٓ
Inna fee thalika laAAibratan limanyakhsha
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
ءَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُ ۚ بَنَىٰهَا
Aantum ashaddu khalqan ami assamaobanaha
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّىٰهَا
RafaAAa samkaha fasawwaha
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَىٰهَا
Waaghtasha laylaha waakhraja duhaha
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
وَٱلْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Wal-arda baAAda thalikadahaha
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
أَخْرَجَ مِنْهَا مَآءَهَا وَمَرْعَىٰهَا
Akhraja minha maahawamarAAaha
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
وَٱلْجِبَالَ أَرْسَىٰهَا
Waljibala arsaha
Na milima akaisimamisha,
مَتَـٰعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَـٰمِكُمْ
MataAAan lakum wali-anAAamikum
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلْكُبْرَىٰ
Fa-itha jaati attammatualkubra
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
يَوْمَ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَـٰنُ مَا سَعَىٰ
Yawma yatathakkaru al-insanu masaAAa
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Waburrizati aljaheemu liman yara
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Faamma man tagha
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
وَءَاثَرَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا
Waathara alhayata addunya
Na akakhiari maisha ya dunia,
فَإِنَّ ٱلْجَحِيمَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ
Fa-inna aljaheema hiya alma/wa
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفْسَ عَنِ ٱلْهَوَىٰ
Waama man khafa maqamarabbihi wanaha annafsa AAani alhawa
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
فَإِنَّ ٱلْجَنَّةَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ
Fa-inna aljannata hiya alma/wa
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
يَسْـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَىٰهَا
Yas-aloonaka AAani assaAAatiayyana mursaha
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَىٰهَآ
Feema anta min thikraha
Una nini wewe hata uitaje?
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Ila rabbika muntahaha
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَىٰهَا
Innama anta munthiru manyakhshaha
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوٓا۟ إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَىٰهَا
Kaannahum yawma yarawnaha lamyalbathoo illa AAashiyyatan aw duhaha
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.