عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
AAamma yatasaaloon
WANAULIZANA nini?
The Tidings
عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
AAamma yatasaaloon
WANAULIZANA nini?
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلْعَظِيمِ
AAani annaba-i alAAatheem
Ile khabari kuu,
ٱلَّذِى هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ
Allathee hum feehi mukhtalifoon
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Kalla sayaAAlamoon
La! Karibu watakuja jua.
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Thumma kalla sayaAAlamoon
Tena la! Karibu watakuja jua.
أَلَمْ نَجْعَلِ ٱلْأَرْضَ مِهَـٰدًا
Alam najAAali al-arda mihada
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
وَٱلْجِبَالَ أَوْتَادًا
Waljibala awtada
Na milima kama vigingi?
وَخَلَقْنَـٰكُمْ أَزْوَٰجًا
Wakhalaqnakum azwaja
Na tukakuumbeni kwa jozi?
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًا
WajaAAalna nawmakum subata
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
وَجَعَلْنَا ٱلَّيْلَ لِبَاسًا
WajaAAalna allayla libasa
Na tukaufanya usiku ni nguo?
وَجَعَلْنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشًا
WajaAAalna annaharamaAAasha
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًا شِدَادًا
Wabanayna fawqakum sabAAan shidada
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
وَجَعَلْنَا سِرَاجًا وَهَّاجًا
WajaAAalna sirajan wahhaja
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
وَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلْمُعْصِرَٰتِ مَآءً ثَجَّاجًا
Waanzalna mina almuAAsiratimaan thajjaja
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
لِّنُخْرِجَ بِهِۦ حَبًّا وَنَبَاتًا
Linukhrija bihi habban wanabata
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
وَجَنَّـٰتٍ أَلْفَافًا
Wajannatin alfafa
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
إِنَّ يَوْمَ ٱلْفَصْلِ كَانَ مِيقَـٰتًا
Inna yawma alfasli kana meeqata
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
يَوْمَ يُنفَخُ فِى ٱلصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًا
Yawma yunfakhu fee assoorifata/toona afwaja
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتْ أَبْوَٰبًا
Wafutihati assamao fakanatabwaba
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
وَسُيِّرَتِ ٱلْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا
Wasuyyirati aljibalu fakanatsaraba
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا
Inna jahannama kanat mirsada
Hakika Jahannamu inangojea!
لِّلطَّـٰغِينَ مَـَٔابًا
Littagheena maaba
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
لَّـٰبِثِينَ فِيهَآ أَحْقَابًا
Labitheena feeha ahqaba
Wakae humo karne baada ya karne,
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا
La yathooqoona feehabardan wala sharaba
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا
Illa hameeman waghassaqa
Ila maji yamoto sana na usaha,
جَزَآءً وِفَاقًا
Jazaan wifaqa
Ndio jaza muwafaka.
إِنَّهُمْ كَانُوا۟ لَا يَرْجُونَ حِسَابًا
Innahum kanoo la yarjoona hisaba
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
وَكَذَّبُوا۟ بِـَٔايَـٰتِنَا كِذَّابًا
Wakaththaboo bi-ayatinakiththaba
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
وَكُلَّ شَىْءٍ أَحْصَيْنَـٰهُ كِتَـٰبًا
Wakulla shay-in ahsaynahu kitaba
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
فَذُوقُوا۟ فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا
Fathooqoo falan nazeedakum illaAAathaba
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا
Inna lilmuttaqeena mafaza
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
حَدَآئِقَ وَأَعْنَـٰبًا
Hada-iqa waaAAnaba
Mabustani na mizabibu,
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا
WakawaAAiba atraba
Na wake walio lingana nao,
وَكَأْسًا دِهَاقًا
Waka/san dihaqa
Na bilauri zilizo jaa,
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّٰبًا
La yasmaAAoona feeha laghwanwala kiththaba
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
جَزَآءً مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابًا
Jazaan min rabbika AAataan hisaba
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
رَّبِّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ٱلرَّحْمَـٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًا
Rabbi assamawati wal-ardiwama baynahuma arrahmani layamlikoona minhu khitaba
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
يَوْمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلْمَلَـٰٓئِكَةُ صَفًّا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحْمَـٰنُ وَقَالَ صَوَابًا
Yawma yaqoomu arroohu walmala-ikatusaffan la yatakallamoona illa man athinalahu arrahmanu waqala sawaba
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلْحَقُّ ۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Thalika alyawmu alhaqqu famanshaa ittakhatha ila rabbihi maaba
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
إِنَّآ أَنذَرْنَـٰكُمْ عَذَابًا قَرِيبًا يَوْمَ يَنظُرُ ٱلْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلْكَافِرُ يَـٰلَيْتَنِى كُنتُ تُرَٰبًۢا
Inna antharnakum AAathabanqareeban yawma yanthuru almaro ma qaddamatyadahu wayaqoolu alkafiru ya laytanee kuntuturaba
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!