وَٱلشَّمْسِ وَضُحَىٰهَا
Washshamsi waduhaha
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
The Sun
وَٱلشَّمْسِ وَضُحَىٰهَا
Washshamsi waduhaha
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
وَٱلْقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Walqamari itha talaha
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Wannahari itha jallaha
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰهَا
Wallayli itha yaghshaha
Na kwa usiku unapo lifunika!
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Wassama-i wama banaha
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
وَٱلْأَرْضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Wal-ardi wama tahaha
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّىٰهَا
Wanafsin wama sawwaha
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَىٰهَا
Faalhamaha fujooraha wataqwaha
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Qad aflaha man zakkaha
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Waqad khaba man dassaha
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَىٰهَآ
Kaththabat thamoodu bitaghwaha
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشْقَىٰهَا
Ithi inbaAAatha ashqaha
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقْيَـٰهَا
Faqala lahum rasoolu Allahi naqataAllahi wasuqyaha
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمْ فَسَوَّىٰهَا
Fakaththaboohu faAAaqaroohafadamdama AAalayhim rabbuhum bithanbihim fasawwaha
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
وَلَا يَخَافُ عُقْبَـٰهَا
Wala yakhafu AAuqbaha
Wala Yeye haogopi matokeo yake.