وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ
Wallayli itha yaghsha
Naapa kwa usiku unapo funika!
The Night
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ
Wallayli itha yaghsha
Naapa kwa usiku unapo funika!
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Wannahari itha tajalla
Na mchana unapo dhihiri!
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ
Wama khalaqa aththakarawal-ontha
Na kwa Aliye umba dume na jike!
إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ
Inna saAAyakum lashatta
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Faamma man aAAta wattaqa
Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
وَصَدَّقَ بِٱلْحُسْنَىٰ
Wasaddaqa bilhusna
Na akaliwafiki lilio jema,
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْيُسْرَىٰ
Fasanuyassiruhu lilyusra
Tutamsahilishia yawe mepesi.
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسْتَغْنَىٰ
Waamma man bakhila wastaghna
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
وَكَذَّبَ بِٱلْحُسْنَىٰ
Wakaththaba bilhusna
Na akakanusha lilio jema,
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْعُسْرَىٰ
Fasanuyassiruhu lilAAusra
Tutamsahilishia yawe mazito!
وَمَا يُغْنِى عَنْهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Wama yughnee AAanhu maluhu ithataradda
Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
إِنَّ عَلَيْنَا لَلْهُدَىٰ
Inna AAalayna lalhuda
Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
وَإِنَّ لَنَا لَلْـَٔاخِرَةَ وَٱلْأُولَىٰ
Wa-inna lana lal-akhirata wal-oola
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
فَأَنذَرْتُكُمْ نَارًا تَلَظَّىٰ
Faanthartukum naran talaththa
Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
لَا يَصْلَىٰهَآ إِلَّا ٱلْأَشْقَى
La yaslaha illaal-ashqa
Hatauingia ila mwovu kabisa!
ٱلَّذِى كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Allathee kaththaba watawalla
Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلْأَتْقَى
Wasayujannabuha al-atqa
Na mchamngu ataepushwa nao,
ٱلَّذِى يُؤْتِى مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Allathee yu/tee malahuyatazakka
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعْمَةٍ تُجْزَىٰٓ
Wama li-ahadin AAindahu minniAAmatin tujza
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
إِلَّا ٱبْتِغَآءَ وَجْهِ رَبِّهِ ٱلْأَعْلَىٰ
Illa ibtighaa wajhi rabbihial-aAAla
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ
Walasawfa yarda
Naye atakuja ridhika!