وَٱلضُّحَىٰ
Wadduha
Naapa kwa mchana!
The Morning Hours
وَٱلضُّحَىٰ
Wadduha
Naapa kwa mchana!
وَٱلَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ
Wallayli itha saja
Na kwa usiku unapo tanda!
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Ma waddaAAaka rabbuka wama qala
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
وَلَلْـَٔاخِرَةُ خَيْرٌ لَّكَ مِنَ ٱلْأُولَىٰ
Walal-akhiratu khayrun laka minaal-oola
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰٓ
Walasawfa yuAAteeka rabbuka fatarda
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًا فَـَٔاوَىٰ
Alam yajidka yateeman faawa
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
وَوَجَدَكَ ضَآلًّا فَهَدَىٰ
Wawajadaka dallan fahada
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
وَوَجَدَكَ عَآئِلًا فَأَغْنَىٰ
Wawajadaka AAa-ilan faaghna
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
فَأَمَّا ٱلْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ
Faamma alyateema fala taqhar
Basi yatima usimwonee!
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنْهَرْ
Waamma assa-ila falatanhar
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ
Waamma biniAAmati rabbika fahaddith
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.