لَآ أُقْسِمُ بِهَـٰذَا ٱلْبَلَدِ
La oqsimu bihatha albalad
Naapa kwa Mji huu!
The City
لَآ أُقْسِمُ بِهَـٰذَا ٱلْبَلَدِ
La oqsimu bihatha albalad
Naapa kwa Mji huu!
وَأَنتَ حِلٌّۢ بِهَـٰذَا ٱلْبَلَدِ
Waanta hillun bihatha albalad
Nawe unaukaa Mji huu.
وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ
Wawalidin wama walad
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَـٰنَ فِى كَبَدٍ
Laqad khalaqna al-insana feekabad
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ
Ayahsabu an lan yaqdira AAalayhi ahad
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُّبَدًا
Yaqoolu ahlaktu malan lubada
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Ayahsabu an lam yarahu ahad
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
أَلَمْ نَجْعَل لَّهُۥ عَيْنَيْنِ
Alam najAAal lahu AAaynayn
Kwani hatukumpa macho mawili?
وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ
Walisanan washafatayn
Na ulimi, na midomo miwili?
وَهَدَيْنَـٰهُ ٱلنَّجْدَيْنِ
Wahadaynahu annajdayn
Na tukambainishia zote njia mbili?
فَلَا ٱقْتَحَمَ ٱلْعَقَبَةَ
Fala iqtahama alAAaqaba
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْعَقَبَةُ
Wama adraka maalAAaqaba
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
فَكُّ رَقَبَةٍ
Fakku raqaba
Kumkomboa mtumwa;
أَوْ إِطْعَـٰمٌ فِى يَوْمٍ ذِى مَسْغَبَةٍ
Aw itAAamun fee yawmin theemasghaba
Au kumlisha siku ya njaa
يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ
Yateeman tha maqraba
Yatima aliye jamaa,
أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ
Aw miskeenan tha matraba
Au masikini aliye vumbini.
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْمَرْحَمَةِ
Thumma kana mina allatheena amanoowatawasaw bissabri watawasaw bilmarhama
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
أُو۟لَـٰٓئِكَ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ
Ola-ika as-habualmaymana
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
وَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ بِـَٔايَـٰتِنَا هُمْ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ
Wallatheena kafaroo bi-ayatinahum as-habu almash-ama
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
عَلَيْهِمْ نَارٌ مُّؤْصَدَةٌۢ
AAalayhim narun mu/sada
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.