وَٱلْفَجْرِ
Walfajr
Naapa kwa alfajiri,
The Dawn
وَٱلْفَجْرِ
Walfajr
Naapa kwa alfajiri,
وَلَيَالٍ عَشْرٍ
Walayalin AAashr
Na kwa masiku kumi,
وَٱلشَّفْعِ وَٱلْوَتْرِ
WashshafAAi walwatr
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَسْرِ
Wallayli itha yasr
Na kwa usiku unapo pita,
هَلْ فِى ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِى حِجْرٍ
Hal fee thalika qasamun lithee hijr
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Alam tara kayfa faAAala rabbuka biAAad
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
إِرَمَ ذَاتِ ٱلْعِمَادِ
Irama thati alAAimad
Wa Iram, wenye majumba marefu?
ٱلَّتِى لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِى ٱلْبِلَـٰدِ
Allatee lam yukhlaq mithluha fee albilad
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُوا۟ ٱلصَّخْرَ بِٱلْوَادِ
Wathamooda allatheena jaboo assakhrabilwad
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
وَفِرْعَوْنَ ذِى ٱلْأَوْتَادِ
WafirAAawna thee al-awtad
Na Firauni mwenye vigingi?
ٱلَّذِينَ طَغَوْا۟ فِى ٱلْبِلَـٰدِ
Allatheena taghaw fee albilad
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
فَأَكْثَرُوا۟ فِيهَا ٱلْفَسَادَ
Faaktharoo feeha alfasad
Wakakithirisha humo ufisadi?
فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ
Fasabba AAalayhim rabbuka sawtaAAathab
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلْمِرْصَادِ
Inna rabbaka labilmirsad
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
فَأَمَّا ٱلْإِنسَـٰنُ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكْرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَكْرَمَنِ
Faamma al-insanu itha maibtalahu rabbuhu faakramahu wanaAAAAamahu fayaqoolu rabbeeakraman
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَهَـٰنَنِ
Waamma itha ma ibtalahufaqadara AAalayhi rizqahu fayaqoolu rabbee ahanan
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ ٱلْيَتِيمَ
Kalla bal la tukrimoonaalyateem
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
وَلَا تَحَـٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ
Wala tahaddoona AAala taAAamialmiskeen
Wala hamhimizani kulisha masikini;
وَتَأْكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا
Wata/kuloona atturatha aklanlamma
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
وَتُحِبُّونَ ٱلْمَالَ حُبًّا جَمًّا
Watuhibboona almala hubbanjamma
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
كَلَّآ إِذَا دُكَّتِ ٱلْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا
Kalla itha dukkati al-ardudakkan dakka
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا
Wajaa rabbuka walmalaku saffansaffa
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
وَجِا۟ىٓءَ يَوْمَئِذٍۭ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَـٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكْرَىٰ
Wajee-a yawma-ithin bijahannamayawma-ithin yatathakkaru al-insanu waannalahu aththikra
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
يَقُولُ يَـٰلَيْتَنِى قَدَّمْتُ لِحَيَاتِى
Yaqoolu ya laytanee qaddamtu lihayatee
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٌ
Fayawma-ithin la yuAAaththibuAAathabahu ahad
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٌ
Wala yoothiqu wathaqahu ahad
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفْسُ ٱلْمُطْمَئِنَّةُ
Ya ayyatuha annafsualmutma-inna
Ewe nafsi iliyo tua!
ٱرْجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً
IrjiAAee ila rabbiki radiyatanmardiyya
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
فَٱدْخُلِى فِى عِبَـٰدِى
Fadkhulee fee AAibadee
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
وَٱدْخُلِى جَنَّتِى
Wadkhulee jannatee
Na ingia katika Pepo yangu.