وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ
Wassama-i thatialburooj
Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
The Mansions of the Stars
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ
Wassama-i thatialburooj
Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
وَٱلْيَوْمِ ٱلْمَوْعُودِ
Walyawmi almawAAood
Na kwa siku iliyo ahidiwa!
وَشَاهِدٍ وَمَشْهُودٍ
Washahidin wamashhood
Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
قُتِلَ أَصْحَـٰبُ ٱلْأُخْدُودِ
Qutila as-habu alukhdood
Wameangamizwa watu wa makhandaki
ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلْوَقُودِ
Annari thati alwaqood
Yenye moto wenye kuni nyingi,
إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌ
Ith hum AAalayha quAAood
Walipo kuwa wamekaa hapo,
وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِٱلْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌ
Wahum AAala ma yafAAaloona bilmu/mineenashuhood
Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
وَمَا نَقَمُوا۟ مِنْهُمْ إِلَّآ أَن يُؤْمِنُوا۟ بِٱللَّهِ ٱلْعَزِيزِ ٱلْحَمِيدِ
Wama naqamoo minhum illa anyu/minoo billahi alAAazeezi alhameed
Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
ٱلَّذِى لَهُۥ مُلْكُ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَىْءٍ شَهِيدٌ
Allathee lahu mulku assamawatiwal-ardi wallahu AAala kullishay-in shaheed
Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُوا۟ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَـٰتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا۟ فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ ٱلْحَرِيقِ
Inna allatheena fatanoo almu/mineenawalmu/minati thumma lam yatooboo falahum AAathabujahannama walahum AAathabu alhareeq
Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ لَهُمْ جَنَّـٰتٌ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَـٰرُ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْفَوْزُ ٱلْكَبِيرُ
Inna allatheena amanoowaAAamiloo assalihati lahum jannatuntajree min tahtiha al-anharu thalikaalfawzu alkabeer
Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
Inna batsha rabbika lashadeed
Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
إِنَّهُۥ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ
Innahu huwa yubdi-o wayuAAeed
Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
وَهُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلْوَدُودُ
Wahuwa alghafooru alwadood
Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
ذُو ٱلْعَرْشِ ٱلْمَجِيدُ
Thoo alAAarshi almajeed
Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
فَعَّالٌ لِّمَا يُرِيدُ
FaAAAAalun lima yureed
Atendaye ayatakayo.
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْجُنُودِ
Hal ataka hadeethu aljunood
Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ
FirAAawna wathamood
Ya Firauni na Thamudi?
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ فِى تَكْذِيبٍ
Bali allatheena kafaroo fee taktheeb
Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطٌۢ
Wallahu min wara-ihimmuheet
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
بَلْ هُوَ قُرْءَانٌ مَّجِيدٌ
Bal huwa qur-anun majeed
Bali hii ni Qur'ani tukufu
فِى لَوْحٍ مَّحْفُوظٍۭ
Fee lawhin mahfooth
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.