ٱلرَّحْمَـٰنُ
Arrahman
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
The Beneficent
ٱلرَّحْمَـٰنُ
Arrahman
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
عَلَّمَ ٱلْقُرْءَانَ
AAallama alqur-an
Amefundisha Qur'ani.
خَلَقَ ٱلْإِنسَـٰنَ
Khalaqa al-insan
Amemuumba mwanaadamu,
عَلَّمَهُ ٱلْبَيَانَ
AAallamahu albayan
Akamfundisha kubaini.
ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ بِحُسْبَانٍ
Ashshamsu walqamaru bihusban
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
وَٱلنَّجْمُ وَٱلشَّجَرُ يَسْجُدَانِ
Wannajmu washshajaru yasjudan
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلْمِيزَانَ
Wassamaa rafaAAahawawadaAAa almeezan
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
أَلَّا تَطْغَوْا۟ فِى ٱلْمِيزَانِ
Alla tatghaw fee almeezan
Ili msidhulumu katika mizani.
وَأَقِيمُوا۟ ٱلْوَزْنَ بِٱلْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا۟ ٱلْمِيزَانَ
Waaqeemoo alwazna bilqisti walatukhsiroo almeezan
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
وَٱلْأَرْضَ وَضَعَهَا لِلْأَنَامِ
Wal-arda wadaAAahalil-anam
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
فِيهَا فَـٰكِهَةٌ وَٱلنَّخْلُ ذَاتُ ٱلْأَكْمَامِ
Feeha fakihatun wannakhluthatu al-akmam
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
وَٱلْحَبُّ ذُو ٱلْعَصْفِ وَٱلرَّيْحَانُ
Walhabbu thoo alAAasfiwarrayhan
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
خَلَقَ ٱلْإِنسَـٰنَ مِن صَلْصَـٰلٍ كَٱلْفَخَّارِ
Khalaqa al-insana min salsalinkalfakhkhar
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
وَخَلَقَ ٱلْجَآنَّ مِن مَّارِجٍ مِّن نَّارٍ
Wakhalaqa aljanna min marijinmin nar
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
رَبُّ ٱلْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ ٱلْمَغْرِبَيْنِ
Rabbu almashriqayni warabbu almaghribayn
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مَرَجَ ٱلْبَحْرَيْنِ يَلْتَقِيَانِ
Maraja albahrayni yaltaqiyan
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
بَيْنَهُمَا بَرْزَخٌ لَّا يَبْغِيَانِ
Baynahuma barzakhun la yabghiyan
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يَخْرُجُ مِنْهُمَا ٱللُّؤْلُؤُ وَٱلْمَرْجَانُ
Yakhruju minhuma allu/luo walmarjan
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththibani
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
وَلَهُ ٱلْجَوَارِ ٱلْمُنشَـَٔاتُ فِى ٱلْبَحْرِ كَٱلْأَعْلَـٰمِ
Walahu aljawari almunshaatufee albahri kal-aAAlam
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ
Kullu man AAalayha fan
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو ٱلْجَلَـٰلِ وَٱلْإِكْرَامِ
Wayabqa wajhu rabbika thooaljalali wal-ikram
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يَسْـَٔلُهُۥ مَن فِى ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِى شَأْنٍ
Yas-aluhu man fee assamawatiwal-ardi kulla yawmin huwa fee sha/n
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
سَنَفْرُغُ لَكُمْ أَيُّهَ ٱلثَّقَلَانِ
Sanafrughu lakum ayyuha aththaqalan
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يَـٰمَعْشَرَ ٱلْجِنِّ وَٱلْإِنسِ إِنِ ٱسْتَطَعْتُمْ أَن تَنفُذُوا۟ مِنْ أَقْطَارِ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ فَٱنفُذُوا۟ ۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلْطَـٰنٍ
Ya maAAshara aljinni wal-insiini istataAAtum an tanfuthoo min aqtari assamawatiwal-ardi fanfuthoo la tanfuthoonailla bisultan
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يُرْسَلُ عَلَيْكُمَا شُوَاظٌ مِّن نَّارٍ وَنُحَاسٌ فَلَا تَنتَصِرَانِ
Yursalu AAalaykuma shuwathunmin narin wanuhasun fala tantasiran
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فَإِذَا ٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتْ وَرْدَةً كَٱلدِّهَانِ
Fa-itha inshaqqati assamaofakanat wardatan kaddihan
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُسْـَٔلُ عَن ذَنۢبِهِۦٓ إِنسٌ وَلَا جَآنٌّ
Fayawma-ithin la yus-alu AAan thanbihiinsun wala jan
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يُعْرَفُ ٱلْمُجْرِمُونَ بِسِيمَـٰهُمْ فَيُؤْخَذُ بِٱلنَّوَٰصِى وَٱلْأَقْدَامِ
YuAArafu almujrimoona biseemahumfayu/khathu binnawasee wal-aqdam
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
هَـٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِى يُكَذِّبُ بِهَا ٱلْمُجْرِمُونَ
Hathihi jahannamu allatee yukaththibubiha almujrimoon
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
يَطُوفُونَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ حَمِيمٍ ءَانٍ
Yatoofoona baynaha wabayna hameeminan
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ
Waliman khafa maqama rabbihijannatan
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ذَوَاتَآ أَفْنَانٍ
Thawata afnan
Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا عَيْنَانِ تَجْرِيَانِ
Feehima AAaynani tajriyan
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا مِن كُلِّ فَـٰكِهَةٍ زَوْجَانِ
Feehima min kulli fakihatinzawjan
Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ فُرُشٍۭ بَطَآئِنُهَا مِنْ إِسْتَبْرَقٍ ۚ وَجَنَى ٱلْجَنَّتَيْنِ دَانٍ
Muttaki-eena AAala furushin bata-inuhamin istabraqin wajana aljannatayni dan
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِنَّ قَـٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَآنٌّ
Feehinna qasiratu attarfilam yatmithhunna insun qablahum wala jan
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
كَأَنَّهُنَّ ٱلْيَاقُوتُ وَٱلْمَرْجَانُ
Kaannahunna alyaqootu walmarjan
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
هَلْ جَزَآءُ ٱلْإِحْسَـٰنِ إِلَّا ٱلْإِحْسَـٰنُ
Hal jazao al-ihsani illaal-ihsan
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ
Wamin doonihima jannatan
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مُدْهَآمَّتَانِ
Mudhammatan
Za kijani kibivu.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا عَيْنَانِ نَضَّاخَتَانِ
Feehima AAaynani naddakhatan
Na chemchem mbili zinazo furika.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا فَـٰكِهَةٌ وَنَخْلٌ وَرُمَّانٌ
Feehima fakihatun wanakhlunwarumman
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِنَّ خَيْرَٰتٌ حِسَانٌ
Feehinna khayratun hisan
Humo wamo wanawake wema wazuri.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
حُورٌ مَّقْصُورَٰتٌ فِى ٱلْخِيَامِ
Hoorun maqsooratun feealkhiyam
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَآنٌّ
Lam yatmithhunna insun qablahum walajan
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ رَفْرَفٍ خُضْرٍ وَعَبْقَرِىٍّ حِسَانٍ
Muttaki-eena AAala rafrafin khudrinwaAAabqariyyin hisan
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Fabi-ayyi ala-i rabbikumatukaththiban
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
تَبَـٰرَكَ ٱسْمُ رَبِّكَ ذِى ٱلْجَلَـٰلِ وَٱلْإِكْرَامِ
Tabaraka ismu rabbika theealjalali wal-ikram
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.