إِذَا وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ
Itha waqaAAati alwaqiAAat
Litakapo tukia hilo Tukio
The Inevitable
إِذَا وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ
Itha waqaAAati alwaqiAAat
Litakapo tukia hilo Tukio
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ
Laysa liwaqAAatiha kathiba
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ
Khafidatun rafiAAa
Literemshalo linyanyualo,
إِذَا رُجَّتِ ٱلْأَرْضُ رَجًّا
Itha rujjati al-ardu rajja
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
وَبُسَّتِ ٱلْجِبَالُ بَسًّا
Wabussati aljibalu bassa
Na milima itapo sagwasagwa,
فَكَانَتْ هَبَآءً مُّنۢبَثًّا
Fakanat habaan munbaththa
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
وَكُنتُمْ أَزْوَٰجًا ثَلَـٰثَةً
Wakuntum azwajan thalatha
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
فَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ
Faas-habu almaymanati maas-habu almaymanat
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
وَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ
Waas-habu almash-amati maas-habu almash-amat
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ
Wassabiqoona assabiqoon
Na wa mbele watakuwa mbele.
أُو۟لَـٰٓئِكَ ٱلْمُقَرَّبُونَ
Ola-ika almuqarraboon
Hao ndio watakao karibishwa
فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Fee jannati annaAAeem
Katika Bustani zenye neema.
ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
Thullatun mina al-awwaleen
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَقَلِيلٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ
Waqaleelun mina al-akhireena
Na wachache katika wa mwisho.
عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ
AAala sururin mawdoona
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيْهَا مُتَقَـٰبِلِينَ
Muttaki-eena AAalayha mutaqabileen
Wakiviegemea wakielekeana.
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌ مُّخَلَّدُونَ
Yatoofu AAalayhim wildanunmukhalladoon
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ
Bi-akwabin waabareeqa waka/sinmin maAAeen
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ
La yusaddaAAoona AAanhawala yunzifoon
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
وَفَـٰكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
Wafakihatin mimmayatakhayyaroon
Na matunda wayapendayo,
وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ
Walahmi tayrin mimmayashtahoon
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
وَحُورٌ عِينٌ
Wahoorun AAeen
Na Mahurulaini,
كَأَمْثَـٰلِ ٱللُّؤْلُؤِ ٱلْمَكْنُونِ
Kaamthali allu/lui almaknoon
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
جَزَآءًۢ بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ
Jazaan bima kanooyaAAmaloon
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا
La yasmaAAoona feeha laghwanwala ta/theema
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
إِلَّا قِيلًا سَلَـٰمًا سَلَـٰمًا
Illa qeelan salaman salama
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
وَأَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ
Waas-habu alyameeni maas-habu alyameen
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
فِى سِدْرٍ مَّخْضُودٍ
Fee sidrin makhdood
Katika mikunazi isiyo na miba,
وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ
Watalhin mandood
Na migomba iliyo pangiliwa,
وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ
Wathillin mamdood
Na kivuli kilicho tanda,
وَمَآءٍ مَّسْكُوبٍ
Wama-in maskoob
Na maji yanayo miminika,
وَفَـٰكِهَةٍ كَثِيرَةٍ
Wafakihatin katheera
Na matunda mengi,
لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ
La maqtooAAatin walamamnooAAa
Hayatindikii wala hayakatazwi,
وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ
Wafurushin marfooAAa
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
إِنَّآ أَنشَأْنَـٰهُنَّ إِنشَآءً
Inna ansha/nahunna inshaa
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
فَجَعَلْنَـٰهُنَّ أَبْكَارًا
FajaAAalnahunna abkara
Na tutawafanya vijana,
عُرُبًا أَتْرَابًا
AAuruban atraba
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
لِّأَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ
Li-as-habi alyameen
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
Thullatun mina al-awwaleen
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ
Wathullatun mina al-akhireen
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
وَأَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ
Waas-habu ashshimalima as-habu ashshimal
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
فِى سَمُومٍ وَحَمِيمٍ
Fee samoomin wahameem
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ
Wathillin min yahmoom
Na kivuli cha moshi mweusi,
لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ
La baridin wala kareem
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ
Innahum kanoo qabla thalikamutrafeen
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
وَكَانُوا۟ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلْحِنثِ ٱلْعَظِيمِ
Wakanoo yusirroona AAalaalhinthi alAAatheem
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
وَكَانُوا۟ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
Wakanoo yaqooloona a-itha mitnawakunna turaban waAAithamana-inna lamabAAoothoon
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ
Awa abaona al-awwaloon
Au baba zetu wa zamani?
قُلْ إِنَّ ٱلْأَوَّلِينَ وَٱلْـَٔاخِرِينَ
Qul inna al-awwaleena wal-akhireen
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَـٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
LamajmooAAoona ila meeqatiyawmin maAAloom
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلْمُكَذِّبُونَ
Thumma innakum ayyuha addalloonaalmukaththiboon
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
لَـَٔاكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ
Laakiloona min shajarin min zaqqoom
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ
Famali-oona minha albutoon
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
فَشَـٰرِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ ٱلْحَمِيمِ
Fashariboona AAalayhi mina alhameem
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
فَشَـٰرِبُونَ شُرْبَ ٱلْهِيمِ
Fashariboona shurba alheem
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
هَـٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ ٱلدِّينِ
Hatha nuzuluhum yawma addeen
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
نَحْنُ خَلَقْنَـٰكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ
Nahnu khalaqnakum falawlatusaddiqoon
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
أَفَرَءَيْتُم مَّا تُمْنُونَ
Afaraaytum ma tumnoon
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
ءَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلْخَـٰلِقُونَ
Aantum takhluqoonahu am nahnu alkhaliqoon
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ ٱلْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
Nahnu qaddarna baynakumualmawta wama nahnu bimasbooqeen
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَـٰلَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِى مَا لَا تَعْلَمُونَ
AAala an nubaddila amthalakumwanunshi-akum fee ma la taAAlamoon
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ ٱلنَّشْأَةَ ٱلْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ
Walaqad AAalimtumu annash-ata al-oolafalawla tathakkaroon
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
أَفَرَءَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ
Afaraaytum ma tahruthoon
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
ءَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلزَّٰرِعُونَ
Aantum tazraAAoonahu am nahnu azzariAAoon
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
لَوْ نَشَآءُ لَجَعَلْنَـٰهُ حُطَـٰمًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ
Law nashao lajaAAalnahu hutamanfathaltum tafakkahoon
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
إِنَّا لَمُغْرَمُونَ
Inna lamughramoon
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
Bal nahnu mahroomoon
Bali sisi tumenyimwa.
أَفَرَءَيْتُمُ ٱلْمَآءَ ٱلَّذِى تَشْرَبُونَ
Afaraaytumu almaa allatheetashraboon
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
ءَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ ٱلْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنزِلُونَ
Aantum anzaltumoohu mina almuzni am nahnualmunziloon
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
لَوْ نَشَآءُ جَعَلْنَـٰهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ
Law nashao jaAAalnahu ojajanfalawla tashkuroon
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
أَفَرَءَيْتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِى تُورُونَ
Afaraaytumu annara allateetooroon
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
ءَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَآ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنشِـُٔونَ
Aantum ansha/tum shajarataha am nahnualmunshi-oon
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
نَحْنُ جَعَلْنَـٰهَا تَذْكِرَةً وَمَتَـٰعًا لِّلْمُقْوِينَ
Nahnu jaAAalnaha tathkiratanwamataAAan lilmuqween
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ
Fasabbih bismi rabbika alAAatheem
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
۞ فَلَآ أُقْسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ
Fala oqsimu bimawaqiAAi annujoom
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ
Wa-innahu laqasamun law taAAlamoona AAatheem
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
إِنَّهُۥ لَقُرْءَانٌ كَرِيمٌ
Innahu laqur-anun kareem
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
فِى كِتَـٰبٍ مَّكْنُونٍ
Fee kitabin maknoon
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلْمُطَهَّرُونَ
La yamassuhu illa almutahharoon
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Tanzeelun min rabbi alAAalameen
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَفَبِهَـٰذَا ٱلْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ
Afabihatha alhadeethi antummudhinoon
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ
WatajAAaloona rizqakum annakum tukaththiboon
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
فَلَوْلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلْحُلْقُومَ
Falawla itha balaghati alhulqoom
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ
Waantum heena-ithin tanthuroona
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَـٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ
Wanahnu aqrabu ilayhi minkum walakinla tubsiroon
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
فَلَوْلَآ إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ
Falawla in kuntum ghayra madeeneen
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
تَرْجِعُونَهَآ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ
TarjiAAoonaha in kuntum sadiqeen
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ
Faamma in kana minaalmuqarrabeen
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ
Farawhun warayhanun wajannatunaAAeem
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنْ أَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ
Waamma in kana min as-habialyameen
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
فَسَلَـٰمٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ
Fasalamun laka min as-habialyameen
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ
Waamma in kana mina almukaththibeenaaddalleen
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ
Fanuzulun min hameem
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ
Watasliyatu jaheem
Na kutiwa Motoni.
إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلْيَقِينِ
Inna hatha lahuwa haqqualyaqeen
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ
Fasabbih bismi rabbika alAAatheem
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.