لَآ أُقْسِمُ بِيَوْمِ ٱلْقِيَـٰمَةِ
La oqsimu biyawmi alqiyamat
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
The Resurrection
لَآ أُقْسِمُ بِيَوْمِ ٱلْقِيَـٰمَةِ
La oqsimu biyawmi alqiyamat
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
وَلَآ أُقْسِمُ بِٱلنَّفْسِ ٱللَّوَّامَةِ
Wala oqsimu binnafsi allawwamat
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَـٰنُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُۥ
Ayahsabu al-insanu allannajmaAAa AAithamah
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
بَلَىٰ قَـٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّىَ بَنَانَهُۥ
Bala qadireena AAala annusawwiya bananah
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
بَلْ يُرِيدُ ٱلْإِنسَـٰنُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُۥ
Bal yureedu al-insanu liyafjura amamah
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
يَسْـَٔلُ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلْقِيَـٰمَةِ
Yas-alu ayyana yawmu alqiyama
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
فَإِذَا بَرِقَ ٱلْبَصَرُ
Fa-itha bariqa albasar
Basi jicho litapo dawaa,
وَخَسَفَ ٱلْقَمَرُ
Wakhasafa alqamar
Na mwezi utapo patwa,
وَجُمِعَ ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ
WajumiAAa ashshamsu walqamar
Na likakusanywa jua na mwezi,
يَقُولُ ٱلْإِنسَـٰنُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ ٱلْمَفَرُّ
Yaqoolu al-insanu yawma-ithinayna almafar
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
كَلَّا لَا وَزَرَ
Kalla la wazar
La! Hapana pa kukimbilia!
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمُسْتَقَرُّ
Ila rabbika yawma-ithinalmustaqar
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
يُنَبَّؤُا۟ ٱلْإِنسَـٰنُ يَوْمَئِذٍۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Yunabbao al-insanu yawma-ithinbima qaddama waakhkhar
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
بَلِ ٱلْإِنسَـٰنُ عَلَىٰ نَفْسِهِۦ بَصِيرَةٌ
Bali al-insanu AAala nafsihibaseera
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
Walaw alqa maAAatheerah
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
لَا تُحَرِّكْ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِۦٓ
La tuharrik bihi lisanakalitaAAjala bih
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُۥ وَقُرْءَانَهُۥ
Inna AAalayna jamAAahu waqur-anah
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
فَإِذَا قَرَأْنَـٰهُ فَٱتَّبِعْ قُرْءَانَهُۥ
Fa-itha qara/nahu fattabiAAqur-anah
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُۥ
Thumma inna AAalayna bayanah
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ ٱلْعَاجِلَةَ
Kalla bal tuhibboona alAAajila
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
وَتَذَرُونَ ٱلْـَٔاخِرَةَ
Watatharoona al-akhira
Na mnaacha maisha ya Akhera.
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاضِرَةٌ
Wujoohun yawma-ithin nadira
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌ
Ila rabbiha nathira
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍۭ بَاسِرَةٌ
Wawujoohun yawma-ithin basira
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌ
Tathunnu an yufAAala bihafaqira
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِىَ
Kalla itha balaghati attaraqiy
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍ
Waqeela man raq
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلْفِرَاقُ
Wathanna annahu alfiraq
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
وَٱلْتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Waltaffati assaqu bilssaq
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمَسَاقُ
Ila rabbika yawma-ithin almasaq
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Fala saddaqa wala salla
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
وَلَـٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Walakin kaththaba watawalla
Bali alikanusha, na akageuka.
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
Thumma thahaba ila ahlihiyatamatta
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ
Awla laka faawla
Ole wako, ole wako!
ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰٓ
Thumma awla laka faawla
Kisha Ole wako, ole wako!
أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَـٰنُ أَن يُتْرَكَ سُدًى
Ayahsabu al-insanu an yutrakasuda
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِّن مَّنِىٍّ يُمْنَىٰ
Alam yaku nutfatan min manayyin yumna
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
Thumma kana AAalaqatan fakhalaqafasawwa
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
فَجَعَلَ مِنْهُ ٱلزَّوْجَيْنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ
FajaAAala minhu azzawjayni aththakarawal-ontha
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَـٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحْـِۧىَ ٱلْمَوْتَىٰ
Alaysa thalika biqadirin AAalaan yuhyiya almawta
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?