يَـٰٓأَيُّهَا ٱلْمُدَّثِّرُ
Ya ayyuha almuddaththir
Ewe uliye jigubika!
The Cloaked One
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلْمُدَّثِّرُ
Ya ayyuha almuddaththir
Ewe uliye jigubika!
قُمْ فَأَنذِرْ
Qum faanthir
Simama uonye!
وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ
Warabbaka fakabbir
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ
Wathiyabaka fatahhir
Na nguo zako, zisafishe.
وَٱلرُّجْزَ فَٱهْجُرْ
Warrujza fahjur
Na yaliyo machafu yahame!
وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ
Wala tamnun tastakthir
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
وَلِرَبِّكَ فَٱصْبِرْ
Walirabbika fasbir
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
فَإِذَا نُقِرَ فِى ٱلنَّاقُورِ
Fa-itha nuqira fee annaqoor
Basi litapo pulizwa barugumu,
فَذَٰلِكَ يَوْمَئِذٍ يَوْمٌ عَسِيرٌ
Fathalika yawma-ithin yawmunAAaseer
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
عَلَى ٱلْكَـٰفِرِينَ غَيْرُ يَسِيرٍ
AAala alkafireena ghayruyaseer
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
ذَرْنِى وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًا
Tharnee waman khalaqtu waheeda
Niache peke yangu na niliye muumba;
وَجَعَلْتُ لَهُۥ مَالًا مَّمْدُودًا
WajaAAaltu lahu malan mamdooda
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
وَبَنِينَ شُهُودًا
Wabaneena shuhooda
Na wana wanao onekana,
وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمْهِيدًا
Wamahhadtu lahu tamheeda
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
ثُمَّ يَطْمَعُ أَنْ أَزِيدَ
Thumma yatmaAAu an azeed
Kisha anatumai nimzidishie!
كَلَّآ ۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِـَٔايَـٰتِنَا عَنِيدًا
Kalla innahu kana li-ayatinaAAaneeda
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
سَأُرْهِقُهُۥ صَعُودًا
Saorhiquhu saAAooda
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ
Innahu fakkara waqaddar
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
فَقُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ
Faqutila kayfa qaddar
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
ثُمَّ قُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ
Thumma qutila kayfa qaddar
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
ثُمَّ نَظَرَ
Thumma nathar
Kisha akatazama,
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Thumma AAabasa wabasar
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
ثُمَّ أَدْبَرَ وَٱسْتَكْبَرَ
Thumma adbara wastakbar
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
فَقَالَ إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا سِحْرٌ يُؤْثَرُ
Faqala in hatha illa sihrunyu/thar
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا قَوْلُ ٱلْبَشَرِ
In hatha illa qawlu albashar
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
سَأُصْلِيهِ سَقَرَ
Saosleehi saqar
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سَقَرُ
Wama adraka ma saqar
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
لَا تُبْقِى وَلَا تَذَرُ
La tubqee wala tathar
Haubakishi wala hausazi.
لَوَّاحَةٌ لِّلْبَشَرِ
Lawwahatun lilbashar
Unababua ngozi iwe nyeusi.
عَلَيْهَا تِسْعَةَ عَشَرَ
AAalayha tisAAata AAashar
Juu yake wapo kumi na tisa.
وَمَا جَعَلْنَآ أَصْحَـٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَـٰٓئِكَةً ۙ وَمَا جَعَلْنَا عِدَّتَهُمْ إِلَّا فِتْنَةً لِّلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لِيَسْتَيْقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُوا۟ ٱلْكِتَـٰبَ وَيَزْدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓا۟ إِيمَـٰنًا ۙ وَلَا يَرْتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُوا۟ ٱلْكِتَـٰبَ وَٱلْمُؤْمِنُونَ ۙ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِى قُلُوبِهِم مَّرَضٌ وَٱلْكَـٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَـٰذَا مَثَلًا ۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهْدِى مَن يَشَآءُ ۚ وَمَا يَعْلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَ ۚ وَمَا هِىَ إِلَّا ذِكْرَىٰ لِلْبَشَرِ
Wama jaAAalna as-habaannari illa mala-ikatan wamajaAAalna AAiddatahum illa fitnatan lillatheenakafaroo liyastayqina allatheena ootoo alkitabawayazdada allatheena amanoo eemananwala yartaba allatheena ootoo alkitabawalmu/minoona waliyaqoola allatheena feequloobihim maradun walkafiroona mathaarada Allahu bihatha mathalan kathalikayudillu Allahu man yashao wayahdee man yashaowama yaAAlamu junooda rabbika illa huwa wamahiya illa thikra lilbashar
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
كَلَّا وَٱلْقَمَرِ
Kalla walqamar
Hasha! Naapa kwa mwezi!
وَٱلَّيْلِ إِذْ أَدْبَرَ
Wallayli ith adbar
Na kwa usiku unapo kucha!
وَٱلصُّبْحِ إِذَآ أَسْفَرَ
Wassubhi ithaasfar
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
إِنَّهَا لَإِحْدَى ٱلْكُبَرِ
Innaha la-ihda alkubar
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
نَذِيرًا لِّلْبَشَرِ
Natheeran lilbashar
Ni onyo kwa binaadamu,
لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَتَقَدَّمَ أَوْ يَتَأَخَّرَ
Liman shaa minkum an yataqaddama awyataakhkhar
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
كُلُّ نَفْسٍۭ بِمَا كَسَبَتْ رَهِينَةٌ
Kullu nafsin bima kasabat raheena
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
إِلَّآ أَصْحَـٰبَ ٱلْيَمِينِ
Illa as-haba alyameen
Isipo kuwa watu wa kuliani.
فِى جَنَّـٰتٍ يَتَسَآءَلُونَ
Fee jannatin yatasaaloon
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
عَنِ ٱلْمُجْرِمِينَ
AAani almujrimeen
Khabari za wakosefu:
مَا سَلَكَكُمْ فِى سَقَرَ
Ma salakakum fee saqar
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
قَالُوا۟ لَمْ نَكُ مِنَ ٱلْمُصَلِّينَ
Qaloo lam naku mina almusalleen
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.
وَلَمْ نَكُ نُطْعِمُ ٱلْمِسْكِينَ
Walam naku nutAAimu almiskeen
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلْخَآئِضِينَ
Wakunna nakhoodu maAAa alkha-ideen
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
Wakunna nukaththibu biyawmi addeen
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلْيَقِينُ
Hatta atanaalyaqeen
Mpaka yakini ilipo tufikia.
فَمَا تَنفَعُهُمْ شَفَـٰعَةُ ٱلشَّـٰفِعِينَ
Fama tanfaAAuhum shafaAAatu ashshafiAAeen
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
فَمَا لَهُمْ عَنِ ٱلتَّذْكِرَةِ مُعْرِضِينَ
Fama lahum AAani attathkiratimuAArideen
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
كَأَنَّهُمْ حُمُرٌ مُّسْتَنفِرَةٌ
Kaannahum humurun mustanfira
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
فَرَّتْ مِن قَسْوَرَةٍۭ
Farrat min qaswara
Wanao mkimbia simba!
بَلْ يُرِيدُ كُلُّ ٱمْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُؤْتَىٰ صُحُفًا مُّنَشَّرَةً
Bal yureedu kullu imri-in minhum an yu/tasuhufan munashshara
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
كَلَّا ۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلْـَٔاخِرَةَ
Kalla bal la yakhafoonaal-akhira
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذْكِرَةٌ
Kalla innahu tathkira
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Faman shaa thakarah
Basi anaye taka atakumbuka.
وَمَا يَذْكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ ۚ هُوَ أَهْلُ ٱلتَّقْوَىٰ وَأَهْلُ ٱلْمَغْفِرَةِ
Wama yathkuroona illaan yashaa Allahu huwa ahlu attaqwawaahlu almaghfirat
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.