سَأَلَ سَآئِلٌۢ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ
Saala sa-ilun biAAathabin waqiAA
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
The Ascending Stairways
سَأَلَ سَآئِلٌۢ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ
Saala sa-ilun biAAathabin waqiAA
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
لِّلْكَـٰفِرِينَ لَيْسَ لَهُۥ دَافِعٌ
Lilkafireena laysa lahu dafiAA
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
مِّنَ ٱللَّهِ ذِى ٱلْمَعَارِجِ
Mina Allahi thee almaAAarij
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
تَعْرُجُ ٱلْمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيْهِ فِى يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُۥ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍ
TaAAruju almala-ikatu warroohuilayhi fee yawmin kana miqdaruhu khamseena alfasana
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
فَٱصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلًا
Fasbir sabran jameela
Basi subiri kwa subira njema.
إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُۥ بَعِيدًا
Innahum yarawnahu baAAeeda
Hakika wao wanaiona iko mbali,
وَنَرَىٰهُ قَرِيبًا
Wanarahu qareeba
Na Sisi tunaiona iko karibu.
يَوْمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلْمُهْلِ
Yawma takoonu assamao kalmuhl
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ
Watakoonu aljibalu kalAAihn
Na milima itakuwa kama sufi.
وَلَا يَسْـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا
Wala yas-alu hameemun hameema
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ ٱلْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِى مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍۭ بِبَنِيهِ
Yubassaroonahum yawaddu almujrimu lawyaftadee min AAathabi yawmi-ithin bibaneeh
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
وَصَـٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ
Wasahibatihi waakheeh
Na mkewe, na nduguye,
وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِى تُـْٔوِيهِ
Wafaseelatihi allatee tu/weeh
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
وَمَن فِى ٱلْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنجِيهِ
Waman fee al-ardi jameeAAan thummayunjeeh
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
كَلَّآ ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ
Kalla innaha latha
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
نَزَّاعَةً لِّلشَّوَىٰ
NazzaAAatan lishshawa
Unao babua ngozi ya kichwa!
تَدْعُوا۟ مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ
TadAAoo man adbara watawalla
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰٓ
WajamaAAa faawAAa
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
۞ إِنَّ ٱلْإِنسَـٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا
Inna al-insana khuliqa halooAAa
Hakika mtu ameumbwa na papara.
إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعًا
Itha massahu ashsharrujazooAAa
Inapo mgusa shari hupapatika.
وَإِذَا مَسَّهُ ٱلْخَيْرُ مَنُوعًا
Wa-itha massahu alkhayru manooAAa
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
إِلَّا ٱلْمُصَلِّينَ
Illa almusalleen
Isipo kuwa wanao sali,
ٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَآئِمُونَ
Allatheena hum AAala salatihimda-imoon
Ambao wanadumisha Sala zao,
وَٱلَّذِينَ فِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ مَّعْلُومٌ
Wallatheena fee amwalihimhaqqun maAAloom
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ
Lissa-ili walmahroom
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
Wallatheena yusaddiqoonabiyawmi addeen
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
وَٱلَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ
Wallatheena hum min AAathabirabbihim mushfiqoon
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ
Inna AAathaba rabbihim ghayru ma/moon
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
وَٱلَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَـٰفِظُونَ
Wallatheena hum lifuroojihim hafithoon
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزْوَٰجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَـٰنُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ
Illa AAala azwajihim awma malakat aymanuhum fa-innahum ghayru maloomeen
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
فَمَنِ ٱبْتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُو۟لَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلْعَادُونَ
Famani ibtagha waraa thalikafaola-ika humu alAAadoon
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
وَٱلَّذِينَ هُمْ لِأَمَـٰنَـٰتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَٰعُونَ
Wallatheena hum li-amanatihimwaAAahdihim raAAoon
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَـٰدَٰتِهِمْ قَآئِمُونَ
Wallatheena hum bishahadatihimqa-imoon
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
وَٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ
Wallatheena hum AAala salatihimyuhafithoon
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
أُو۟لَـٰٓئِكَ فِى جَنَّـٰتٍ مُّكْرَمُونَ
Ola-ika fee jannatin mukramoon
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ
Famali allatheena kafarooqibalaka muhtiAAeen
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
عَنِ ٱلْيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ
AAani alyameeni waAAani ashshimaliAAizeen
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
أَيَطْمَعُ كُلُّ ٱمْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ
AyatmaAAu kullu imri-in minhum anyudkhala jannata naAAeem
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
كَلَّآ ۖ إِنَّا خَلَقْنَـٰهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ
Kalla inna khalaqnahummimma yaAAlamoon
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
فَلَآ أُقْسِمُ بِرَبِّ ٱلْمَشَـٰرِقِ وَٱلْمَغَـٰرِبِ إِنَّا لَقَـٰدِرُونَ
Fala oqsimu birabbi almashariqiwalmagharibi inna laqadiroon
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
AAala an nubaddila khayran minhum wamanahnu bimasbooqeen
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا۟ وَيَلْعَبُوا۟ حَتَّىٰ يُلَـٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ
Fatharhum yakhoodoowayalAAaboo hatta yulaqoo yawmahumu allatheeyooAAadoon
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍ يُوفِضُونَ
Yawma yakhrujoona mina al-ajdathi siraAAankaannahum ila nusubin yoofidoon
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
خَـٰشِعَةً أَبْصَـٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلَّذِى كَانُوا۟ يُوعَدُونَ
KhashiAAatan absaruhumtarhaquhum thillatun thalika alyawmu allatheekanoo yooAAadoon
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.