ٱلْحَآقَّةُ
Alhaqqa
Tukio la haki.
The Reality
ٱلْحَآقَّةُ
Alhaqqa
Tukio la haki.
مَا ٱلْحَآقَّةُ
Ma alhaqqa
Nini hilo Tukio la haki?
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْحَآقَّةُ
Wama adraka ma alhaqqa
Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
كَذَّبَتْ ثَمُودُ وَعَادٌۢ بِٱلْقَارِعَةِ
Kaththabat thamoodu waAAadun bilqariAAa
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهْلِكُوا۟ بِٱلطَّاغِيَةِ
Faamma thamoodu faohlikoo bittaghiya
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
وَأَمَّا عَادٌ فَأُهْلِكُوا۟ بِرِيحٍ صَرْصَرٍ عَاتِيَةٍ
Waamma AAadun faohlikoo bireehinsarsarin AAatiya
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
سَخَّرَهَا عَلَيْهِمْ سَبْعَ لَيَالٍ وَثَمَـٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومًا فَتَرَى ٱلْقَوْمَ فِيهَا صَرْعَىٰ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ خَاوِيَةٍ
Sakhkharaha AAalayhim sabAAa layalinwathamaniyata ayyamin husooman fataraalqawma feeha sarAAa kaannahum aAAjazunakhlin khawiya
Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
فَهَلْ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٍ
Fahal tara lahum min baqiya
Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
وَجَآءَ فِرْعَوْنُ وَمَن قَبْلَهُۥ وَٱلْمُؤْتَفِكَـٰتُ بِٱلْخَاطِئَةِ
Wajaa firAAawnu waman qablahu walmu/tafikatubilkhati-a
Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
فَعَصَوْا۟ رَسُولَ رَبِّهِمْ فَأَخَذَهُمْ أَخْذَةً رَّابِيَةً
FaAAasaw rasoola rabbihim faakhathahumakhthatan rabiya
Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلْمَآءُ حَمَلْنَـٰكُمْ فِى ٱلْجَارِيَةِ
Inna lamma taghaalmao hamalnakum fee aljariya
Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
لِنَجْعَلَهَا لَكُمْ تَذْكِرَةً وَتَعِيَهَآ أُذُنٌ وَٰعِيَةٌ
LinajAAalaha lakum tathkiratanwataAAiyaha othunun waAAiya
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
فَإِذَا نُفِخَ فِى ٱلصُّورِ نَفْخَةٌ وَٰحِدَةٌ
Fa-itha nufikha fee assoorinafkhatun wahida
Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
وَحُمِلَتِ ٱلْأَرْضُ وَٱلْجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةً وَٰحِدَةً
Wahumilati al-ardu waljibalufadukkata dakkatan wahida
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
فَيَوْمَئِذٍ وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ
Fayawma-ithin waqaAAati alwaqiAAa
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِىَ يَوْمَئِذٍ وَاهِيَةٌ
Wanshaqqati assamaofahiya yawma-ithin wahiya
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
وَٱلْمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرْجَآئِهَا ۚ وَيَحْمِلُ عَرْشَ رَبِّكَ فَوْقَهُمْ يَوْمَئِذٍ ثَمَـٰنِيَةٌ
Walmalaku AAala arja-ihawayahmilu AAarsha rabbika fawqahum yawma-ithin thamaniya
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
يَوْمَئِذٍ تُعْرَضُونَ لَا تَخْفَىٰ مِنكُمْ خَافِيَةٌ
Yawma-ithin tuAAradoona latakhfa minkum khafiya
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
فَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَـٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقْرَءُوا۟ كِتَـٰبِيَهْ
Faamma man ootiya kitabahubiyameenihi fayaqoolu haomu iqraoo kitabiyah
Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
إِنِّى ظَنَنتُ أَنِّى مُلَـٰقٍ حِسَابِيَهْ
Innee thanantu annee mulaqinhisabiyah
Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
فَهُوَ فِى عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ
Fahuwa fee AAeeshatin radiya
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍ
Fee jannatin AAaliya
Katika Bustani ya juu,
قُطُوفُهَا دَانِيَةٌ
Qutoofuha daniya
Matunda yake yakaribu.
كُلُوا۟ وَٱشْرَبُوا۟ هَنِيٓـًٔۢا بِمَآ أَسْلَفْتُمْ فِى ٱلْأَيَّامِ ٱلْخَالِيَةِ
Kuloo washraboo hanee-an bimaaslaftum fee al-ayyami alkhaliya
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
وَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَـٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَـٰلَيْتَنِى لَمْ أُوتَ كِتَـٰبِيَهْ
Waamma man ootiya kitabahubishimalihi fayaqoolu ya laytanee lam oota kitabiyah
Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
وَلَمْ أَدْرِ مَا حِسَابِيَهْ
Walam adri ma hisabiyah
Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
يَـٰلَيْتَهَا كَانَتِ ٱلْقَاضِيَةَ
Ya laytaha kanati alqadiya
Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
مَآ أَغْنَىٰ عَنِّى مَالِيَهْ ۜ
Ma aghna AAannee maliyah
Mali yangu hayakunifaa kitu.
هَلَكَ عَنِّى سُلْطَـٰنِيَهْ
Halaka AAannee sultaniyah
Madaraka yangu yamenipotea.
خُذُوهُ فَغُلُّوهُ
Khuthoohu faghullooh
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
ثُمَّ ٱلْجَحِيمَ صَلُّوهُ
Thumma aljaheema sallooh
Kisha mtupeni Motoni!
ثُمَّ فِى سِلْسِلَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعًا فَٱسْلُكُوهُ
Thumma fee silsilatin tharAAuhasabAAoona thiraAAan faslukooh
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!
إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤْمِنُ بِٱللَّهِ ٱلْعَظِيمِ
Innahu kana la yu/minu billahialAAatheem
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ
Wala yahuddu AAalataAAami almiskeen
Wala hahimizi kulisha masikini.
فَلَيْسَ لَهُ ٱلْيَوْمَ هَـٰهُنَا حَمِيمٌ
Falaysa lahu alyawma hahuna hameem
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,
وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنْ غِسْلِينٍ
Wala taAAamun illamin ghisleen
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
لَّا يَأْكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلْخَـٰطِـُٔونَ
La ya/kuluhu illa alkhati-oon
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
فَلَآ أُقْسِمُ بِمَا تُبْصِرُونَ
Fala oqsimu bima tubsiroon
Basi naapa kwa mnavyo viona,
وَمَا لَا تُبْصِرُونَ
Wama la tubsiroon
Na msivyo viona,
إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ
Innahu laqawlu rasoolin kareem
Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَاعِرٍ ۚ قَلِيلًا مَّا تُؤْمِنُونَ
Wama huwa biqawli shaAAirinqaleelan ma tu/minoon
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
وَلَا بِقَوْلِ كَاهِنٍ ۚ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ
Wala biqawli kahinin qaleelanma tathakkaroon
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Tanzeelun min rabbi alAAalameen
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
وَلَوْ تَقَوَّلَ عَلَيْنَا بَعْضَ ٱلْأَقَاوِيلِ
Walaw taqawwala AAalayna baAAdaal-aqaweel
Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
لَأَخَذْنَا مِنْهُ بِٱلْيَمِينِ
Laakhathna minhu bilyameen
Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
ثُمَّ لَقَطَعْنَا مِنْهُ ٱلْوَتِينَ
Thumma laqataAAna minhualwateen
Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
فَمَا مِنكُم مِّنْ أَحَدٍ عَنْهُ حَـٰجِزِينَ
Fama minkum min ahadin AAanhu hajizeen
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
وَإِنَّهُۥ لَتَذْكِرَةٌ لِّلْمُتَّقِينَ
Wa-innahu latathkiratun lilmuttaqeen
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
وَإِنَّا لَنَعْلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ
Wa-inna lanaAAlamu anna minkum mukaththibeen
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.
وَإِنَّهُۥ لَحَسْرَةٌ عَلَى ٱلْكَـٰفِرِينَ
Wa-innahu lahasratun AAala alkafireen
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلْيَقِينِ
Wa-innahu lahaqqu alyaqeen
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ
Fasabbih bismi rabbika alAAatheem
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.