طسٓمٓ
Ta-seen-meem
T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)
The Poets
طسٓمٓ
Ta-seen-meem
T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)
تِلْكَ ءَايَـٰتُ ٱلْكِتَـٰبِ ٱلْمُبِينِ
Tilka ayatu alkitabialmubeen
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
لَعَلَّكَ بَـٰخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
LaAAallaka bakhiAAun nafsaka allayakoonoo mu/mineen
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةً فَظَلَّتْ أَعْنَـٰقُهُمْ لَهَا خَـٰضِعِينَ
In nasha/ nunazzil AAalayhim mina assama-iayatan fathallat aAAnaquhum lahakhadiAAeen
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ ٱلرَّحْمَـٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا۟ عَنْهُ مُعْرِضِينَ
Wama ya/teehim min thikrin minaarrahmani muhdathin illa kanooAAanhu muAArideen
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
فَقَدْ كَذَّبُوا۟ فَسَيَأْتِيهِمْ أَنۢبَـٰٓؤُا۟ مَا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ
Faqad kaththaboo fasaya/teehim anbaoma kanoo bihi yastahzi-oon
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
أَوَلَمْ يَرَوْا۟ إِلَى ٱلْأَرْضِ كَمْ أَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ
Awa lam yaraw ila al-ardi kamanbatna feeha min kulli zawjin kareem
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatan wamakana aktharuhum mu/mineen
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئْتِ ٱلْقَوْمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ
Wa-ith nada rabbukamoosa ani i/ti alqawma aththalimeen
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
قَوْمَ فِرْعَوْنَ ۚ أَلَا يَتَّقُونَ
Qawma firAAawna ala yattaqoon
Watu wa Firauni. Hawaogopi?
قَالَ رَبِّ إِنِّىٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Qala rabbi innee akhafu anyukaththiboon
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
وَيَضِيقُ صَدْرِى وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِى فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَـٰرُونَ
Wayadeequ sadree walayantaliqu lisanee faarsil ila haroon
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
وَلَهُمْ عَلَىَّ ذَنۢبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ
Walahum AAalayya thanbun faakhafuan yaqtuloon
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
قَالَ كَلَّا ۖ فَٱذْهَبَا بِـَٔايَـٰتِنَآ ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ
Qala kalla fathhababi-ayatina inna maAAakum mustamiAAoon
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Fa/tiya firAAawna faqoola innarasoolu rabbi alAAalameen
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
An arsil maAAana banee isra-eel
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ
Qala alam nurabbika feenawaleedan walabithta feena min AAumurika sineen
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ ٱلَّتِى فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلْكَـٰفِرِينَ
WafaAAalta faAAlataka allatee faAAaltawaanta mina alkafireen
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?
قَالَ فَعَلْتُهَآ إِذًا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
Qala faAAaltuha ithanwaana mina addalleen
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِى رَبِّى حُكْمًا وَجَعَلَنِى مِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Fafarartu minkum lamma khiftukumfawahaba lee rabbee hukman wajaAAalanee mina almursaleen
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَىَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
Watilka niAAmatun tamunnuha AAalayyaan AAabbadta banee isra-eel
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Qala firAAawnu wama rabbu alAAalameen
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Qala rabbu assamawatiwal-ardi wama baynahuma in kuntummooqineen
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُۥٓ أَلَا تَسْتَمِعُونَ
Qala liman hawlahu alatastamiAAoon
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
Qala rabbukum warabbu aba-ikumual-awwaleen
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِىٓ أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ
Qala inna rasoolakumu allatheeorsila ilaykum lamajnoon
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
قَالَ رَبُّ ٱلْمَشْرِقِ وَٱلْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ
Qala rabbu almashriqi walmaghribiwama baynahuma in kuntum taAAqiloon
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذْتَ إِلَـٰهًا غَيْرِى لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ ٱلْمَسْجُونِينَ
Qala la-ini ittakhathta ilahanghayree laajAAalannaka mina almasjooneen
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَىْءٍ مُّبِينٍ
Qala awa law ji/tuka bishay-in mubeen
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
قَالَ فَأْتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
Qala fa/ti bihi in kunta mina assadiqeen
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ
Faalqa AAasahu fa-ithahiya thuAAbanun mubeen
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِىَ بَيْضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ
WanazaAAa yadahu fa-itha hiya baydaolinnathireen
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُۥٓ إِنَّ هَـٰذَا لَسَـٰحِرٌ عَلِيمٌ
Qala lilmala-i hawlahu inna hathalasahirun AAaleem
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِۦ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ
Yureedu an yukhrijakum min ardikumbisihrihi famatha ta/muroon
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
قَالُوٓا۟ أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَٱبْعَثْ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَـٰشِرِينَ
Qaloo arjih waakhahu wabAAathfee almada-ini hashireen
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍ
Ya/tooka bikulli sahharin AAaleem
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَـٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
FajumiAAa assaharatu limeeqatiyawmin maAAloom
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ
Waqeela linnasi hal antummujtamiAAoon
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
LaAAallana nattabiAAu assaharatain kanoo humu alghalibeen
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُوا۟ لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
Falamma jaa assaharatuqaloo lifirAAawna a-inna lana laajran in kunnanahnu alghalibeen
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?
قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ
Qala naAAam wa-innakum ithanlamina almuqarrabeen
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلْقُوا۟ مَآ أَنتُم مُّلْقُونَ
Qala lahum moosa alqoo maantum mulqoon
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
فَأَلْقَوْا۟ حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا۟ بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ ٱلْغَـٰلِبُونَ
Faalqaw hibalahum waAAisiyyahumwaqaloo biAAizzati firAAawna inna lanahnualghaliboon
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ
Faalqa moosa AAasahufa-itha hiya talqafu ma ya/fikoon
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
فَأُلْقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سَـٰجِدِينَ
Faolqiya assaharatu sajideen
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
قَالُوٓا۟ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Qaloo amanna birabbialAAalameen
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
Rabbi moosa waharoon
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
قَالَ ءَامَنتُمْ لَهُۥ قَبْلَ أَنْ ءَاذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِى عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَـٰفٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ
Qala amantum lahu qabla an athanalakum innahu lakabeerukumu allathee AAallamakumu assihrafalasawfa taAAlamoona laoqattiAAanna aydiyakum waarjulakummin khilafin walaosallibannakum ajmaAAeen
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
قَالُوا۟ لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Qaloo la dayra innaila rabbina munqaliboon
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَـٰيَـٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Inna natmaAAu an yaghfira lanarabbuna khatayana an kunnaawwala almu/mineen
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.
۞ وَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِىٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Waawhayna ila moosaan asri biAAibadee innakum muttabaAAoon
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَـٰشِرِينَ
Faarsala firAAawnu fee almada-ini hashireen
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ
Inna haola-i lashirthimatunqaleeloon
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَآئِظُونَ
Wa-innahum lana lagha-ithoon
Nao wanatuudhi.
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَـٰذِرُونَ
Wa-inna lajameeAAun hathiroon
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
فَأَخْرَجْنَـٰهُم مِّن جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
Faakhrajnahum min jannatinwaAAuyoon
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
وَكُنُوزٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ
Wakunoozin wamaqamin kareem
Na makhazina, na vyeo vya hishima,
كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَـٰهَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
Kathalika waawrathnahabanee isra-eel
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ
FaatbaAAoohum mushriqeen
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَـٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ
Falamma taraa aljamAAaniqala as-habu moosa innalamudrakoon
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!
قَالَ كَلَّآ ۖ إِنَّ مَعِىَ رَبِّى سَيَهْدِينِ
Qala kalla inna maAAiya rabbeesayahdeen
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
فَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضْرِب بِّعَصَاكَ ٱلْبَحْرَ ۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَٱلطَّوْدِ ٱلْعَظِيمِ
Faawhayna ila moosaani idrib biAAasaka albahra fanfalaqafakana kullu firqin kattawdi alAAatheem
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ ٱلْـَٔاخَرِينَ
Waazlafna thamma al-akhareen
Na tukawajongeza hapo wale wengine.
وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
Waanjayna moosa waman maAAahuajmaAAeen
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Thumma aghraqna al-akhareen
Kisha tukawazamisha hao wengine.
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatan wamakana aktharuhum mu/mineen
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
وَٱتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَٰهِيمَ
Watlu AAalayhim nabaa ibraheem
Na wasomee khabari za Ibrahim.
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَا تَعْبُدُونَ
Ith qala li-abeehi waqawmihi mataAAbudoon
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
قَالُوا۟ نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَـٰكِفِينَ
Qaloo naAAbudu asnamanfanathallu laha AAakifeen
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ
Qala hal yasmaAAoonakum ithtadAAoon
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ
Aw yanfaAAoonakum aw yadurroon
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?
قَالُوا۟ بَلْ وَجَدْنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ
Qaloo bal wajadna abaanakathalika yafAAaloon
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
قَالَ أَفَرَءَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Qala afaraaytum ma kuntumtaAAbudoon
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-
أَنتُمْ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلْأَقْدَمُونَ
Antum waabaokumu al-aqdamoon
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّىٓ إِلَّا رَبَّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Fa-innahum AAaduwwun lee illa rabbaalAAalameen
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ٱلَّذِى خَلَقَنِى فَهُوَ يَهْدِينِ
Allathee khalaqanee fahuwa yahdeen
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
وَٱلَّذِى هُوَ يُطْعِمُنِى وَيَسْقِينِ
Wallathee huwa yutAAimuneewayasqeen
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ
Wa-itha maridtu fahuwayashfeen
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
وَٱلَّذِى يُمِيتُنِى ثُمَّ يُحْيِينِ
Wallathee yumeetunee thummayuhyeen
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
وَٱلَّذِىٓ أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِى خَطِيٓـَٔتِى يَوْمَ ٱلدِّينِ
Wallathee atmaAAu anyaghfira lee khatee-atee yawma addeen
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
رَبِّ هَبْ لِى حُكْمًا وَأَلْحِقْنِى بِٱلصَّـٰلِحِينَ
Rabbi hab lee hukman waalhiqneebissaliheen
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
وَٱجْعَل لِّى لِسَانَ صِدْقٍ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
WajAAal lee lisana sidqinfee al-akhireen
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
وَٱجْعَلْنِى مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ
WajAAalnee min warathati jannati annaAAeem
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
وَٱغْفِرْ لِأَبِىٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
Waghfir li-abee innahu kanamina addalleen
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
وَلَا تُخْزِنِى يَوْمَ يُبْعَثُونَ
Wala tukhzinee yawma yubAAathoon
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ
Yawma la yanfaAAu malun walabanoon
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
إِلَّا مَنْ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Illa man ata Allahabiqalbin saleem
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
وَأُزْلِفَتِ ٱلْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ
Waozlifati aljannatu lilmuttaqeen
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ
Waburrizati aljaheemu lilghaween
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Waqeela lahum ayna ma kuntumtaAAbudoon
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ
Min dooni Allahi hal yansuroonakumaw yantasiroon
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
فَكُبْكِبُوا۟ فِيهَا هُمْ وَٱلْغَاوُۥنَ
Fakubkiboo feeha hum walghawoon
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ
Wajunoodu ibleesa ajmaAAoon
Na majeshi ya Ibilisi yote.
قَالُوا۟ وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ
Qaloo wahum feeha yakhtasimoon
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِى ضَلَـٰلٍ مُّبِينٍ
Tallahi in kunna lafeedalalin mubeen
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Ith nusawweekum birabbi alAAalameen
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلْمُجْرِمُونَ
Wama adallana illaalmujrimoon
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.
فَمَا لَنَا مِن شَـٰفِعِينَ
Fama lana min shafiAAeen
Basi hatuna waombezi.
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ
Wala sadeeqin hameem
Wala rafiki wa dhati.
فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Falaw anna lana karratan fanakoonamina almu/mineen
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatan wamakana aktharuhum mu/mineen
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ ٱلْمُرْسَلِينَ
Kaththabat qawmu noohinalmursaleen
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Ith qala lahum akhoohum noohunala tattaqoon
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Innee lakum rasoolun ameen
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Wama as-alukum AAalayhi min ajrin inajriya illa AAala rabbi alAAalameen
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
۞ قَالُوٓا۟ أَنُؤْمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلْأَرْذَلُونَ
Qaloo anu/minu laka wattabaAAakaal-arthaloon
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
قَالَ وَمَا عِلْمِى بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ
Qala wama AAilmee bimakanoo yaAAmaloon
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّى ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ
In hisabuhum illa AAalarabbee law tashAAuroon
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Wama ana bitaridialmu/mineen
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
إِنْ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
In ana illa natheerunmubeen
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَـٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمَرْجُومِينَ
Qaloo la-in lam tantahi yanoohu latakoonanna mina almarjoomeen
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِى كَذَّبُونِ
Qala rabbi inna qawmee kaththaboon
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
فَٱفْتَحْ بَيْنِى وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِى وَمَن مَّعِىَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Faftah baynee wabaynahum fathanwanajjinee waman maAAiya mina almu/mineen
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.
فَأَنجَيْنَـٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
Faanjaynahu waman maAAahu feealfulki almashhoon
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.
ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ ٱلْبَاقِينَ
Thumma aghraqna baAAdu albaqeen
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatan wamakana aktharuhum mu/mineen
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
كَذَّبَتْ عَادٌ ٱلْمُرْسَلِينَ
Kaththabat AAadun almursaleen
Kina A'd waliwakanusha Mitume.
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Ith qala lahum akhoohumhoodun ala tattaqoon
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Innee lakum rasoolun ameen
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Wama as-alukum AAalayhi min ajrin inajriya illa AAala rabbi alAAalameen
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةً تَعْبَثُونَ
Atabnoona bikulli reeAAin ayatantaAAbathoon
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ
Watattakhithoona masaniAAalaAAallakum takhludoon
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!
وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ
Wa-itha batashtum batashtumjabbareen
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِىٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ
Wattaqoo allathee amaddakumbima taAAlamoon
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.
أَمَدَّكُم بِأَنْعَـٰمٍ وَبَنِينَ
Amaddakum bi-anAAamin wabaneen
Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.
وَجَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
Wajannatin waAAuyoon
Na mabustani na chemchem.
إِنِّىٓ أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Innee akhafu AAalaykum AAathabayawmin AAatheem
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.
قَالُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْنَآ أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ ٱلْوَٰعِظِينَ
Qaloo sawaon AAalaynaawaAAathta am lam takun mina alwaAAitheen
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلْأَوَّلِينَ
In hatha illa khuluqual-awwaleen
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Wama nahnu bimuAAaththabeen
Wala sisi hatutaadhibiwa.
فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَـٰهُمْ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Fakaththaboohu faahlaknahuminna fee thalika laayatan wama kanaaktharuhum mu/mineen
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
كَذَّبَتْ ثَمُودُ ٱلْمُرْسَلِينَ
Kaththabat thamoodu almursaleen
Kina Thamud waliwakanusha Mitume.
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَـٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Ith qala lahum akhoohum salihunala tattaqoon
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Innee lakum rasoolun ameen
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Wama as-alukum AAalayhi min ajrin inajriya illa AAala rabbi alAAalameen
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَتُتْرَكُونَ فِى مَا هَـٰهُنَآ ءَامِنِينَ
Atutrakoona fee ma hahunaamineen
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
Fee jannatin waAAuyoon
Katika mabustani, na chemchem?
وَزُرُوعٍ وَنَخْلٍ طَلْعُهَا هَضِيمٌ
WazurooAAin wanakhlin talAAuhahadeem
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.
وَتَنْحِتُونَ مِنَ ٱلْجِبَالِ بُيُوتًا فَـٰرِهِينَ
Watanhitoona mina aljibalibuyootan fariheen
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
وَلَا تُطِيعُوٓا۟ أَمْرَ ٱلْمُسْرِفِينَ
Wala tuteeAAoo amraalmusrifeen
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,
ٱلَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِى ٱلْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ
Allatheena yufsidoona fee al-ardiwala yuslihoon
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.
قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ
Qaloo innama anta mina almusahhareen
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.
مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
Ma anta illa basharun mithlunafa/ti bi-ayatin in kunta mina assadiqeena
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
قَالَ هَـٰذِهِۦ نَاقَةٌ لَّهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
Qala hathihi naqatunlaha shirbun walakum shirbu yawmin maAAloom
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Wala tamassooha bisoo-infaya/khuthakum AAathabu yawmin AAatheem
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.
فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا۟ نَـٰدِمِينَ
FaAAaqarooha faasbahoonadimeen
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.
فَأَخَذَهُمُ ٱلْعَذَابُ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Faakhathahumu alAAathabu innafee thalika laayatan wama kanaaktharuhum mu/mineen
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ ٱلْمُرْسَلِينَ
Kaththabat qawmu lootinalmursaleen
Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Ith qala lahum akhoohum lootunala tattaqoon
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Innee lakum rasoolun ameen
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Wama as-alukum AAalayhi min ajrin inajriya illa AAala rabbi alAAalameen
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَتَأْتُونَ ٱلذُّكْرَانَ مِنَ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Ata/toona aththukranamina alAAalameen
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَٰجِكُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ
Watatharoona ma khalaqa lakumrabbukum min azwajikum bal antum qawmun AAadoon
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!
قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَـٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمُخْرَجِينَ
Qaloo la-in lam tantahi yalootu latakoonanna mina almukhrajeen
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!
قَالَ إِنِّى لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلْقَالِينَ
Qala innee liAAamalikum mina alqaleen
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.
رَبِّ نَجِّنِى وَأَهْلِى مِمَّا يَعْمَلُونَ
Rabbi najjinee waahlee mimmayaAAmaloon
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
فَنَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
Fanajjaynahu waahlahu ajmaAAeen
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,
إِلَّا عَجُوزًا فِى ٱلْغَـٰبِرِينَ
Illa AAajoozan fee alghabireen
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.
ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Thumma dammarna al-akhareen
Kisha tukawaangamiza wale wengine.
وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا ۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلْمُنذَرِينَ
Waamtarna AAalayhim mataranfasaa mataru almunthareen
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatan wamakana aktharuhum mu/mineen
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
كَذَّبَ أَصْحَـٰبُ لْـَٔيْكَةِ ٱلْمُرْسَلِينَ
Kaththaba as-habual-aykati almursaleen
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Ith qala lahum shuAAaybun alatattaqoon
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Innee lakum rasoolun ameen
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Fattaqoo Allaha waateeAAoon
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Wama as-alukum AAalayhi min ajrin inajriya illa AAala rabbi alAAalameen
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
۞ أَوْفُوا۟ ٱلْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا۟ مِنَ ٱلْمُخْسِرِينَ
Awfoo alkayla wala takoonoo minaalmukhsireen
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.
وَزِنُوا۟ بِٱلْقِسْطَاسِ ٱلْمُسْتَقِيمِ
Wazinoo bilqistasialmustaqeem
Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;
وَلَا تَبْخَسُوا۟ ٱلنَّاسَ أَشْيَآءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا۟ فِى ٱلْأَرْضِ مُفْسِدِينَ
Wala tabkhasoo annasaashyaahum wala taAAthaw fee al-ardimufsideen
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.
وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِى خَلَقَكُمْ وَٱلْجِبِلَّةَ ٱلْأَوَّلِينَ
Wattaqoo allathee khalaqakumwaljibillata al-awwaleen
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.
قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ
Qaloo innama anta mina almusahhareen
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.
وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلْكَـٰذِبِينَ
Wama anta illa basharunmithluna wa-in nathunnuka lamina alkathibeen
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
Faasqit AAalayna kisafan minaassama-i in kunta mina assadiqeen
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
قَالَ رَبِّىٓ أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ
Qala rabbee aAAlamu bimataAAmaloon
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ ٱلظُّلَّةِ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Fakaththaboohu faakhathahumAAathabu yawmi aththullati innahu kanaAAathaba yawmin AAatheem
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Inna fee thalika laayatan wamakana aktharuhum mu/mineen
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu arraheem
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Wa-innahu latanzeelu rabbi alAAalameen
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلْأَمِينُ
Nazala bihi arroohu al-ameen
Ameuteremsha Roho muaminifu,
عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلْمُنذِرِينَ
AAala qalbika litakoona mina almunthireen
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,
بِلِسَانٍ عَرَبِىٍّ مُّبِينٍ
Bilisanin AAarabiyyin mubeen
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
وَإِنَّهُۥ لَفِى زُبُرِ ٱلْأَوَّلِينَ
Wa-innahu lafee zuburi al-awwaleen
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ ءَايَةً أَن يَعْلَمَهُۥ عُلَمَـٰٓؤُا۟ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
Awa lam yakun lahum ayatan anyaAAlamahu AAulamao banee isra-eel
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?
وَلَوْ نَزَّلْنَـٰهُ عَلَىٰ بَعْضِ ٱلْأَعْجَمِينَ
Walaw nazzalnahu AAala baAAdial-aAAjameen
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,
فَقَرَأَهُۥ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا۟ بِهِۦ مُؤْمِنِينَ
Faqaraahu AAalayhim ma kanoobihi mu/mineen
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.
كَذَٰلِكَ سَلَكْنَـٰهُ فِى قُلُوبِ ٱلْمُجْرِمِينَ
Kathalika salaknahu feequloobi almujrimeen
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.
لَا يُؤْمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُا۟ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ
La yu/minoona bihi hattayarawoo alAAathaba al-aleem
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ
Faya/tiyahum baghtatan wahum layashAAuroon
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.
فَيَقُولُوا۟ هَلْ نَحْنُ مُنظَرُونَ
Fayaqooloo hal nahnu muntharoon
Na watasema: Je, tutapewa muhula?
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
AfabiAAathabina yastaAAjiloon
Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?
أَفَرَءَيْتَ إِن مَّتَّعْنَـٰهُمْ سِنِينَ
Afaraayta in mattaAAnahum sineen
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,
ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُوا۟ يُوعَدُونَ
Thumma jaahum ma kanooyooAAadoon
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,
مَآ أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا۟ يُمَتَّعُونَ
Ma aghna AAanhum ma kanooyumattaAAoon
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?
وَمَآ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
Wama ahlakna min qaryatin illalaha munthiroon
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -
ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَـٰلِمِينَ
Thikra wama kunnathalimeen
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ ٱلشَّيَـٰطِينُ
Wama tanazzalat bihi ashshayateen
Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,
وَمَا يَنۢبَغِى لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ
Wama yanbaghee lahum wamayastateeAAoon
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
إِنَّهُمْ عَنِ ٱلسَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ
Innahum AAani assamAAilamaAAzooloona
Hakika hao wametengwa na kusikia.
فَلَا تَدْعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَـٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلْمُعَذَّبِينَ
Fala tadAAu maAAa Allahi ilahanakhara fatakoona mina almuAAaththabeen
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.
وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ ٱلْأَقْرَبِينَ
Waanthir AAasheerataka al-aqrabeen
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
وَٱخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Wakhfid janahakalimani ittabaAAaka mina almu/mineen
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.
فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّى بَرِىٓءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ
Fa-in AAasawka faqul innee baree-onmimma taAAmaloon
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.
وَتَوَكَّلْ عَلَى ٱلْعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ
Watawakkal AAala alAAazeezi arraheem
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ٱلَّذِى يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ
Allathee yaraka heenataqoom
Ambaye anakuona unapo simama,
وَتَقَلُّبَكَ فِى ٱلسَّـٰجِدِينَ
Wataqallubaka fee assajideen
Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.
إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ
Innahu huwa assameeAAu alAAaleem
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَـٰطِينُ
Hal onabbi-okum AAala man tanazzaluashshayateen
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ
Tanazzalu AAala kulli affakinatheem
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
يُلْقُونَ ٱلسَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَـٰذِبُونَ
Yulqoona assamAAa waaktharuhum kathiboon
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.
وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلْغَاوُۥنَ
WashshuAAaraoyattabiAAuhumu alghawoon
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِى كُلِّ وَادٍ يَهِيمُونَ
Alam tara annahum fee kulli wadinyaheemoon
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ
Waannahum yaqooloona ma layafAAaloon
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ وَذَكَرُوا۟ ٱللَّهَ كَثِيرًا وَٱنتَصَرُوا۟ مِنۢ بَعْدِ مَا ظُلِمُوا۟ ۗ وَسَيَعْلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓا۟ أَىَّ مُنقَلَبٍ يَنقَلِبُونَ
Illa allatheena amanoowaAAamiloo assalihati wathakaroo Allahakatheeran wantasaroo min baAAdi ma thulimoowasayaAAlamu allatheena thalamoo ayyamunqalabin yanqaliboon
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.