وَٱلصَّـٰٓفَّـٰتِ صَفًّا
Wassaffati saffa
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
Those who set the Ranks
وَٱلصَّـٰٓفَّـٰتِ صَفًّا
Wassaffati saffa
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجْرًا
Fazzajirati zajra
Na kwa wenye kukataza mabaya.
فَٱلتَّـٰلِيَـٰتِ ذِكْرًا
Fattaliyati thikra
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
إِنَّ إِلَـٰهَكُمْ لَوَٰحِدٌ
Inna ilahakum lawahid
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
رَّبُّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ ٱلْمَشَـٰرِقِ
Rabbu assamawati wal-ardiwama baynahuma warabbu almashariq
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنْيَا بِزِينَةٍ ٱلْكَوَاكِبِ
Inna zayyanna assamaaaddunya bizeenatin alkawakib
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَـٰنٍ مَّارِدٍ
Wahifthan min kulli shaytaninmarid
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلْمَلَإِ ٱلْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ
La yassammaAAoona ila almala-ial-aAAla wayuqthafoona min kulli janib
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ
Duhooran walahum AAathabun wasib
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
إِلَّا مَنْ خَطِفَ ٱلْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌ ثَاقِبٌ
Illa man khatifa alkhatfatafaatbaAAahu shihabun thaqib
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
فَٱسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَآ ۚ إِنَّا خَلَقْنَـٰهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍۭ
Fastaftihim ahum ashaddu khalqan amman khalaqna inna khalaqnahum min teeninlazib
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ
Bal AAajibta wayaskharoon
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
وَإِذَا ذُكِّرُوا۟ لَا يَذْكُرُونَ
Wa-itha thukkiroo la yathkuroon
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
وَإِذَا رَأَوْا۟ ءَايَةً يَسْتَسْخِرُونَ
Wa-itha raaw ayatanyastaskhiroon
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
وَقَالُوٓا۟ إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
Waqaloo in hatha illasihrun mubeen
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
A-itha mitna wakunnaturaban waAAithaman a-innalamabAAoothoon
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ
Awa abaona al-awwaloon
Hata baba zetu wa zamani?
قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَٰخِرُونَ
Qul naAAam waantum dakhiroon
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌ وَٰحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ
Fa-innama hiya zajratun wahidatunfa-itha hum yanthuroon
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
وَقَالُوا۟ يَـٰوَيْلَنَا هَـٰذَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Waqaloo ya waylana hathayawmu addeen
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
هَـٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Hatha yawmu alfasli allatheekuntum bihi tukaththiboon
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
۞ ٱحْشُرُوا۟ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ وَأَزْوَٰجَهُمْ وَمَا كَانُوا۟ يَعْبُدُونَ
Ohshuroo allatheena thalamoowaazwajahum wama kanoo yaAAbudoon
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلْجَحِيمِ
Min dooni Allahi fahdoohum ilasirati aljaheem
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْـُٔولُونَ
Waqifoohum innahum masooloon
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ
Ma lakum la tanasaroon
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
بَلْ هُمُ ٱلْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ
Bal humu alyawma mustaslimoon
Bali hii leo, watasalimu amri.
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
Waaqbala baAAduhum AAala baAAdinyatasaaloon
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
قَالُوٓا۟ إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ ٱلْيَمِينِ
Qaloo innakum kuntum ta/toonanaAAani alyameen
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
قَالُوا۟ بَل لَّمْ تَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
Qaloo bal lam takoonoo mu/mineen
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَـٰنٍۭ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَـٰغِينَ
Wama kana lanaAAalaykum min sultanin bal kuntum qawman tagheen
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَآ ۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ
Fahaqqa AAalayna qawlu rabbinainna latha-iqoon
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
فَأَغْوَيْنَـٰكُمْ إِنَّا كُنَّا غَـٰوِينَ
Faaghwaynakum inna kunnaghaween
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِى ٱلْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ
Fa-innahum yawma-ithin fee alAAathabimushtarikoon
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ
Inna kathalika nafAAalu bilmujrimeen
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
إِنَّهُمْ كَانُوٓا۟ إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ
Innahum kanoo itha qeela lahumla ilaha illa Allahu yastakbiroon
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓا۟ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍۭ
Wayaqooloona a-inna latarikoo alihatinalishaAAirin majnoon
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
بَلْ جَآءَ بِٱلْحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Bal jaa bilhaqqi wasaddaqaalmursaleen
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
إِنَّكُمْ لَذَآئِقُوا۟ ٱلْعَذَابِ ٱلْأَلِيمِ
Innakum latha-iqoo alAAathabial-aleem
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Wama tujzawna illa makuntum taAAmaloon
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Illa AAibada Allahialmukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
أُو۟لَـٰٓئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ
Ola-ika lahum rizqun maAAloom
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
فَوَٰكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ
Fawakihu wahum mukramoon
Matunda, nao watahishimiwa.
فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Fee jannati annaAAeem
Katika Bustani za neema.
عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَـٰبِلِينَ
AAala sururin mutaqabileen
Wako juu ya viti wamekabiliana.
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍۭ
Yutafu AAalayhim bika/sin min maAAeen
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
بَيْضَآءَ لَذَّةٍ لِّلشَّـٰرِبِينَ
Baydaa laththatin lishsharibeen
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ
La feeha ghawlun walahum AAanha yunzafoon
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
وَعِندَهُمْ قَـٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ عِينٌ
WaAAindahum qasiratu attarfiAAeen
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ
Kaannahunna baydun maknoon
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
Faaqbala baAAduhum AAala baAAdinyatasaaloon
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
قَالَ قَآئِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّى كَانَ لِى قَرِينٌ
Qala qa-ilun minhum innee kanalee qareen
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلْمُصَدِّقِينَ
Yaqoolu a-innaka lamina almusaddiqeen
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ
A-itha mitna wakunnaturaban waAAithaman a-innalamadeenoon
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Qala hal antum muttaliAAoon
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِى سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ
FattalaAAa faraahu feesawa-i aljaheem
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ
Qala tallahi in kidtalaturdeen
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّى لَكُنتُ مِنَ ٱلْمُحْضَرِينَ
Walawla niAAmatu rabbee lakuntu minaalmuhdareen
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ
Afama nahnu bimayyiteen
Je! Sisi hatutakufa,
إِلَّا مَوْتَتَنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Illa mawtatana al-oolawama nahnu bimuAAaththabeen
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ
Inna hatha lahuwa alfawzu alAAatheem
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
لِمِثْلِ هَـٰذَا فَلْيَعْمَلِ ٱلْعَـٰمِلُونَ
Limithli hatha falyaAAmali alAAamiloon
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ
Athalika khayrun nuzulan am shajaratuazzaqqoom
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
إِنَّا جَعَلْنَـٰهَا فِتْنَةً لِّلظَّـٰلِمِينَ
Inna jaAAalnahafitnatan liththalimeen
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِىٓ أَصْلِ ٱلْجَحِيمِ
Innaha shajaratun takhruju fee aslialjaheem
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
طَلْعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَـٰطِينِ
TalAAuha kaannahu ruoosu ashshayateen
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
فَإِنَّهُمْ لَـَٔاكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ
Fa-innahum laakiloona minhafamali-oona minha albutoon
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ
Thumma inna lahum AAalayha lashawbanmin hameem
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى ٱلْجَحِيمِ
Thumma inna marjiAAahum la-ila aljaheem
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
إِنَّهُمْ أَلْفَوْا۟ ءَابَآءَهُمْ ضَآلِّينَ
Innahum alfaw abaahum dalleen
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
فَهُمْ عَلَىٰٓ ءَاثَـٰرِهِمْ يُهْرَعُونَ
Fahum AAala atharihimyuhraAAoon
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ ٱلْأَوَّلِينَ
Walaqad dalla qablahum aktharual-awwaleen
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Walaqad arsalna feehim munthireen
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
فَٱنظُرْ كَيْفَ كَانَ عَـٰقِبَةُ ٱلْمُنذَرِينَ
Fanthur kayfa kanaAAaqibatu almunthareen
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Illa AAibada Allahialmukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
وَلَقَدْ نَادَىٰنَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ ٱلْمُجِيبُونَ
Walaqad nadana noohunfalaniAAma almujeeboon
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
وَنَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥ مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
Wanajjaynahu waahlahu mina alkarbialAAatheem
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلْبَاقِينَ
WajaAAalna thurriyyatahu humualbaqeen
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Watarakna AAalayhi fee al-akhireen
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
سَلَـٰمٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِى ٱلْعَـٰلَمِينَ
Salamun AAala noohinfee alAAalameen
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Inna kathalika najzee almuhsineen
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Innahu min AAibadinaalmu/mineen
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Thumma aghraqna al-akhareen
Kisha tukawazamisha wale wengine.
۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبْرَٰهِيمَ
Wa-inna min sheeAAatihi la-ibraheem
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
إِذْ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Ith jaa rabbahu biqalbinsaleem
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَاذَا تَعْبُدُونَ
Ith qala li-abeehi waqawmihi mathataAAbudoon
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
أَئِفْكًا ءَالِهَةً دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ
A-ifkan alihatan doona Allahitureedoon
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Fama thannukum birabbialAAalameen
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
فَنَظَرَ نَظْرَةً فِى ٱلنُّجُومِ
Fanathara nathratanfee annujoom
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
فَقَالَ إِنِّى سَقِيمٌ
Faqala innee saqeem
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
فَتَوَلَّوْا۟ عَنْهُ مُدْبِرِينَ
Fatawallaw AAanhu mudbireen
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Faragha ila alihatihimfaqala ala ta/kuloon
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ
Ma lakum la tantiqoon
Mna nini hata hamsemi?
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًۢا بِٱلْيَمِينِ
Faragha AAalayhim darban bilyameen
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
فَأَقْبَلُوٓا۟ إِلَيْهِ يَزِفُّونَ
Faaqbaloo ilayhi yaziffoon
Basi wakamjia upesi upesi.
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ
Qala ataAAbudoona ma tanhitoon
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
وَٱللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
Wallahu khalaqakum wamataAAmaloon
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
قَالُوا۟ ٱبْنُوا۟ لَهُۥ بُنْيَـٰنًا فَأَلْقُوهُ فِى ٱلْجَحِيمِ
Qaloo ibnoo lahu bunyananfaalqoohu fee aljaheem
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
فَأَرَادُوا۟ بِهِۦ كَيْدًا فَجَعَلْنَـٰهُمُ ٱلْأَسْفَلِينَ
Faaradoo bihi kaydan fajaAAalnahumual-asfaleen
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
وَقَالَ إِنِّى ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّى سَيَهْدِينِ
Waqala innee thahibun ilarabbee sayahdeen
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
رَبِّ هَبْ لِى مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
Rabbi hablee mina assaliheen
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
فَبَشَّرْنَـٰهُ بِغُلَـٰمٍ حَلِيمٍ
Fabashsharnahu bighulamin haleem
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعْىَ قَالَ يَـٰبُنَىَّ إِنِّىٓ أَرَىٰ فِى ٱلْمَنَامِ أَنِّىٓ أَذْبَحُكَ فَٱنظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَـٰٓأَبَتِ ٱفْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِىٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّـٰبِرِينَ
Falamma balagha maAAahu assaAAyaqala ya bunayya innee ara fee almanamiannee athbahuka fanthur mathatara qala ya abati ifAAal ma tu/marusatajidunee in shaa Allahu mina assabireen
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
فَلَمَّآ أَسْلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلْجَبِينِ
Falamma aslama watallahuliljabeen
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
وَنَـٰدَيْنَـٰهُ أَن يَـٰٓإِبْرَٰهِيمُ
Wanadaynahu an ya ibraheem
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
قَدْ صَدَّقْتَ ٱلرُّءْيَآ ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Qad saddaqta arru/yainna kathalika najzee almuhsineen
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ ٱلْبَلَـٰٓؤُا۟ ٱلْمُبِينُ
Inna hatha lahuwa albalaoalmubeen
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
وَفَدَيْنَـٰهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ
Wafadaynahu bithibhinAAatheem
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Watarakna AAalayhi fee al-akhireen
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
سَلَـٰمٌ عَلَىٰٓ إِبْرَٰهِيمَ
Salamun AAala ibraheem
Iwe salama kwa Ibrahim!
كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Kathalika najzee almuhsineen
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Innahu min AAibadinaalmu/mineen
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
وَبَشَّرْنَـٰهُ بِإِسْحَـٰقَ نَبِيًّا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
Wabashsharnahu bi-ishaqanabiyyan mina assaliheen
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
وَبَـٰرَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰٓ إِسْحَـٰقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِۦ مُبِينٌ
Wabarakna AAalayhi waAAalaishaqa wamin thurriyyatihima muhsinunwathalimun linafsihi mubeen
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
Walaqad mananna AAala moosawaharoon
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
وَنَجَّيْنَـٰهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
Wanajjaynahuma waqawmahumamina alkarbi alAAatheem
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
وَنَصَرْنَـٰهُمْ فَكَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
Wanasarnahum fakanoohumu alghalibeen
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
وَءَاتَيْنَـٰهُمَا ٱلْكِتَـٰبَ ٱلْمُسْتَبِينَ
Waataynahuma alkitabaalmustabeen
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
وَهَدَيْنَـٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ
Wahadaynahuma assirataalmustaqeem
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Watarakna AAalayhima fee al-akhireen
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
سَلَـٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
Salamun AAala moosawaharoon
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Inna kathalika najzee almuhsineen
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Innahuma min AAibadinaalmu/mineen
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Wa-inna ilyasa lamina almursaleen
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ
Ith qala liqawmihi alatattaqoon
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ ٱلْخَـٰلِقِينَ
AtadAAoona baAAlan watatharoona ahsanaalkhaliqeen
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
ٱللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
Allaha rabbakum warabba aba-ikumual-awwaleen
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
Fakaththaboohu fa-innahum lamuhdaroon
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Illa AAibada Allahialmukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Watarakna AAalayhi fee al-akhireen
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
سَلَـٰمٌ عَلَىٰٓ إِلْ يَاسِينَ
Salamun AAala il yaseen
Iwe salama kwa Ilyas.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Inna kathalika najzee almuhsineen
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Innahu min AAibadinaalmu/mineen
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Wa-inna lootan lamina almursaleen
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
إِذْ نَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
Ith najjaynahu waahlahuajmaAAeen
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
إِلَّا عَجُوزًا فِى ٱلْغَـٰبِرِينَ
Illa AAajoozan fee alghabireen
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Thumma dammarna al-akhareen
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ
Wa-innakum latamurroona AAalayhim musbiheen
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
وَبِٱلَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
Wabillayli afala taAAqiloon
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Wa-inna yoonusa lamina almursaleen
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
إِذْ أَبَقَ إِلَى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
Ith abaqa ila alfulki almashhoon
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلْمُدْحَضِينَ
Fasahama fakana mina almudhadeen
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
فَٱلْتَقَمَهُ ٱلْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ
Faltaqamahu alhootu wahuwamuleem
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
فَلَوْلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلْمُسَبِّحِينَ
Falawla annahu kana minaalmusabbiheen
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
لَلَبِثَ فِى بَطْنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
Lalabitha fee batnihi ilayawmi yubAAathoon
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
۞ فَنَبَذْنَـٰهُ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٌ
Fanabathnahu bilAAara-iwahuwa saqeem
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
وَأَنۢبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ
Waanbatna AAalayhi shajaratan minyaqteen
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
وَأَرْسَلْنَـٰهُ إِلَىٰ مِا۟ئَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ
Waarsalnahu ila mi-ati alfinaw yazeedoon
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
فَـَٔامَنُوا۟ فَمَتَّعْنَـٰهُمْ إِلَىٰ حِينٍ
Faamanoo famattaAAnahum ilaheen
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
فَٱسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ ٱلْبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلْبَنُونَ
Fastaftihim alirabbika albanatuwalahumu albanoon
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
أَمْ خَلَقْنَا ٱلْمَلَـٰٓئِكَةَ إِنَـٰثًا وَهُمْ شَـٰهِدُونَ
Am khalaqna almala-ikata inathanwahum shahidoon
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
أَلَآ إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ
Ala innahum min ifkihim layaqooloon
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَـٰذِبُونَ
Walada Allahu wa-innahum lakathiboon
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
أَصْطَفَى ٱلْبَنَاتِ عَلَى ٱلْبَنِينَ
Astafa albanati AAalaalbaneen
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
Ma lakum kayfa tahkumoon
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
Afala tathakkaroon
Hamkumbuki?
أَمْ لَكُمْ سُلْطَـٰنٌ مُّبِينٌ
Am lakum sultanun mubeen
Au mnayo hoja iliyo wazi?
فَأْتُوا۟ بِكِتَـٰبِكُمْ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ
Fa/too bikitabikum in kuntum sadiqeen
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
وَجَعَلُوا۟ بَيْنَهُۥ وَبَيْنَ ٱلْجِنَّةِ نَسَبًا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ ٱلْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
WajaAAaloo baynahu wabayna aljinnatinasaban walaqad AAalimati aljinnatu innahum lamuhdaroon
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
سُبْحَـٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
Subhana Allahi AAammayasifoon
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Illa AAibada Allahialmukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ
Fa-innakum wama taAAbudoon
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
مَآ أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَـٰتِنِينَ
Ma antum AAalayhi bifatineen
Hamwezi kuwapoteza
إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ ٱلْجَحِيمِ
Illa man huwa sali aljaheem
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ
Wama minna illa lahumaqamun maAAloom
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلصَّآفُّونَ
Wa-inna lanahnu assaffoon
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلْمُسَبِّحُونَ
Wa-inna lanahnu almusabbihoon
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
وَإِن كَانُوا۟ لَيَقُولُونَ
Wa-in kanoo layaqooloon
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
Law anna AAindana thikranmina al-awwaleen
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Lakunna AAibada Allahialmukhlaseen
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
فَكَفَرُوا۟ بِهِۦ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Fakafaroo bihi fasawfa yaAAlamoon
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلْمُرْسَلِينَ
Walaqad sabaqat kalimatuna liAAibadinaalmursaleen
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
إِنَّهُمْ لَهُمُ ٱلْمَنصُورُونَ
Innahum lahumu almansooroon
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلْغَـٰلِبُونَ
Wa-inna jundana lahumu alghaliboon
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
Fatawalla AAanhum hatta heen
Basi waachilie mbali kwa muda.
وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Waabsirhum fasawfa yubsiroon
Na watazame, nao wataona.
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
AfabiAAathabina yastaAAjiloon
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلْمُنذَرِينَ
Fa-itha nazala bisahatihimfasaa sabahu almunthareen
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
Watawalla AAanhum hatta heen
Na waache kwa muda.
وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Waabsir fasawfa yubsiroon
Na tazama, na wao wataona.
سُبْحَـٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
Subhana rabbika rabbi alAAizzatiAAamma yasifoon
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
وَسَلَـٰمٌ عَلَى ٱلْمُرْسَلِينَ
Wasalamun AAala almursaleen
Na Salamu juu ya Mitume.
وَٱلْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Walhamdu lillahirabbi alAAalameen
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.